Google PlusRSS FeedEmail
 Diwani wa Kata ya Msongola, Ukonga, Dar es Salaam, Angel Malembeka (kulia) ameipiga tafu timu ya soka ya Uhuru FM, kwa kuipatia jozi mbili za jezi na mipira miwili ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano baina ya timu hiyo na kata yake. Pichani, Diwani huyo akikabidhi vifaa kwa uongozi wa timu hiyo, Angel Alikimali na Furaha Luhende, katika hafla fupi iliyofanyika nje ya Jengo la CCM mkoa wa Dar es Salaam, leo. Wakati Luhende ni Mwenyekiti wa timu hiyo,  Akilimali ambaye ni Kaimu Mkurugebzi Mtendaji wa Uhuru FM ni mlezi wa timu hiyo.
 Akilimali akimshukuru Masala Mabula ambaye ni mchezaji aliyeibuliwa kipaji chake katika michuano ya Malembeka Cup iliyomalizika hivi karibuni ambaye sasa anajiandaa kwenda Msumbiji kucheza soka la kulipwa. Masala alifuatrana na Diwani huyo (kulia)
Luhende na Akilimali wakifurahia vifaa hivyo baada ya kukabidhiwa na diwani
 Diwani na Akilimali wakiwa na baadhi ya waandishi na watangazaji wa Uhuru baada ya makabidhiano hayo.
Mtangazaji wa Uhuru FM, Mhina Dungumalo akimhoji diwani huyo baada ya makabidhiano Imetayarishwa na theNkoromo Blog

DIWANI MALEMBEKA AIPIGA JEKI TIMU YA SOKA YA UHURU FM

 Diwani wa Kata ya Msongola, Ukonga, Dar es Salaam, Angel Malembeka (kulia) ameipiga tafu timu ya soka ya Uhuru FM, kwa kuipatia jozi mbili ... [Read More]

ZANZIBAR, Tanzania
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaongoza viongozi na mamia ya wananchi wa Zanzibar katika mazishi ya mwanasiasa na mwanadiplomasia mkongwe Balozi Issac Abraham Sepetu yaliyofanyika huko kijijini kwake Mbuzini, Wilaya ya Magharibi Mkoa wa Mjini Magharibi unguja.  
Serikali katika salamu zake zilitolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Mohamed Aboud Mohamed imesema kuwa Marehemu Balozi Sepetu atabaki katika nyoyo za wananchi wa Zanzibar na Tanzania kwa jumla kutokana na mchango wake katika kulitumikia Taifa.  
Waziri Aboud alimuelezea Balozi Sepetu ambaye katika uhai wake alishika nafasi mbali mbali katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuwa mtu aliyeitumika nchi yake kwa uadilifu na uaminifu mkubwa hivyo msiba huo si wa familia tu bali kwa wananchi wote wa Zanzibar na Tanzania.  
Alisema Serikali na wananchi wa Zanzibar wamepokea kwa masikitiko makubwa msiba wa hayati Balozi Sepetu na kuwaomba wanafamilia kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki kigumu cha maombolezi.  
Akitoa salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mazishi hayo  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe alisema Rais Jakaya Mrisho wa Kikwete ameguswa sana na kifo cha Balozi Sepetu ambaye aliwahi kufanya nae kazi katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa miaka kumi.  
Alisema kifo chake ni pigo kwa taifa na daima watanzania watamkumbuka sana Balozi Sepetu na kubaki katika nyoyo zao kutokana na utumishi wake bora kwa taifa.  
Akisoma wasifu wa Balozi Sepetu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitega Uchumi-ZIPA nchini Khamis Salum alieleza kuwa maraeehmu Balozi Sepetu alizaliwa tarehe 16 Oktoba, 1943 huko Tabora alipata elimu yake ya msingi na sekondari katika skuli ya Mtakatifu Joseph mjini Unguja ambayo sasa inaitwa Tumekuja.  
Mwaka 1966 alikwenda iliyokuwa Ujerumani Mashariki kwa masomo hadi mwaka 1970 ambapo alihitimu shahada ya pili katika Uchumi na sayansi ya siasa. Aliporejea nyumbani aliteuliwa kushika nafasi ya Meneja Msaidizi Mkuu wa Shirika la Shirika la Biashara Zanzibar BIZANJE.  
Kabla ya kwenda masomoni nchini Ujerumani marehemu alifanyakazi katika Idara ya Habari na Utangazaji Zanzibar na aliwahi kuwa Mhariri Msaidizi wa Gazeti la Kweupe ambalo llianzishwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar Marehemu Abeid Amani Karume.    
Balozi wa Sepetu aliwahi kushika nyadhifa za Naibu wa Waziri wa Mambo ya Nje, Waziri wa Habari na Utalii katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi wa Tanzania katika Shirikisho la nchi za Kisoshalisti la Kisovieti wakati huo na Jamhuri ya Kidemkrasia ya Kongo wakati huo ikiitwa Zaire.  
Katika Serikali ya Zanzibar aliwahi kuwa Kamishna wa Tume ya Mipango, Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Mipango.Mwaka 2000 alichaguliwa mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki hadi mwaka 2005. Hadi anaaga dunia Balozi Sepetu alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya ZIPA.  
Marehemu Balozi Sepetu ameacha wajane wawili, watoto na wajukuu.    
Mazishi hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad na Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi pamoja na wageni mbalibali kutoka Tanzania bara. 
wakati huo huo mamia ya wakaazi wa mji wa Zanzibar walitoa heshma zao za mwisho kwa mwili wa marehemu Balozi Issac Abraham Sepetu mapema asubuhi huko katika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi uliopo mjini Unguja
Mwili wa marehemu uliwasili kwa boti mapema asubuhi ukitokea Dar es Salaam ambako Balozi Sepetu mauti yalimkuta.
Baadae mwili ulipelekwa katika Kanisa la Roma la Minara Miwili lililopo Shangani mjini hapa kwa misa.

BALOZI SEPETU AZIKWA ZANZIBAR LEO

ZANZIBAR, Tanzania Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein leo amewaongoza viongozi na mamia ya wananchi... [Read More]

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua rasmi kongamano la kujadili Mtandao wa maji kwa Nchi Wanachama wa SADC, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, leoJijini Dar es Salaam.
  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua rasmi kongamano la kujadili Mtandao wa maji kwa Nchi Wanachama wa SADC, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, leoJijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa 'local Organizing Commitee', Prof. Mtalo Felix, akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kongamano hilo.
  Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi.
   Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi.
   Baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa Kongamano hilo baada ya kufungua rasmi
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Bashir Mrindoko, wakati akiondoka baada ya picha ya pamoja na kufungua Kongamano la kujadili Mtandao wa maji kwa Nchi Wanachama wa SADC, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, leoJijini dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano huo, Prof. Mtalo Felix, wakati akiondoka baada ya picha ya pamoja na kufungua Kongamano la kujadili Mtandao wa maji kwa Nchi Wanachama wa SADC, lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, leoJijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS AFUNGUA KONGAMANO KUJADILI MTANDAO WA MAJI KWA NCHI8 ZA SADC

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua rasmi kongamano la kujadili Mtandao wa maji kwa Nc... [Read More]

DAR ES SALAAM, Tanzania
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Rais Mstaafu wa Shirikisho la Mpira nchini (TFF) Leodegar Tenga kwa uongozi wa kupigiwa mfano uliowezesha kuleta mapinduzi katika mifumo wa mchezo wa soka nchini.

Pia imemtumia salam za pongezi Rais Mpya wa TFF, Jamal Malinzi, na Uongozi wake wote mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) uliopatikana katika uchaguzi uliofanyika juzi, Oktoba 27, 2013 jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam, leo, na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi, Nape Nnauye inasema Chama hicho kinaimani kubwa na Malinzi wa wenzake katika kuendeleza jitihada zilizoanzishwa na uongozi uliomaliza muda wake sanjari na kuibua mbinu mpya zitakazoboresha na kuleta mapinduzi makubwa ya soka nchini.

Katika taarifa hiyo, Nape ameuasa uongozi mpya kujiepusha na jitihada za kujiendeleza binafsi na badala yake uwekeze katika soka na kuepusha migogoro isiyo na tija katika mchezo huo ambao kwa sasa ndio unaopendwa na Watanzania wengi.

“Daima imani huzaa imani, hivyo imani ya CCM kwako (Malinzi) na kwa viongozi wenzako mliochaguliwa pamoja izae imani ya utumishi uliotukuka" alisema  Nape.

Nape amesema Chama Cha Mapinduzi kinatambua kuwa migogoro imekuwa kwa sehemu kubwa chanzo cha kukwamisha sana maendeleo ya soka hapa nchini na hivyo kuwanyima Watanzania raha ambayo huitarajia kutoka kwenye mchezo huo na hasa pale timu zao zinapopata ushindi.

CCM YAWAPONGEZA MALINZI, TENGA

DAR ES SALAAM, Tanzania Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempongeza Rais Mstaafu wa Shirikisho la Mpira nchini (TFF) Leodegar Tenga kwa uongozi w... [Read More]

 Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha-Rose Migiro, akimpongeza Kada wa CCM, Asha Abdallah Juma, baada ya kumtunuku shahada ya pili ya Biashara ya Chuo hicho, katika mahafali ya 25, yaliyofanyika leo, Makao Makuu ya OUT, Bungo, Kibaha mkoa wa Pwani. Kushoto ni Makamnu Mkuu  wa Chuo hicho, Profesa Tolly Mbwette. Asha ambaye sasa ni Mjumbe wa NEC CCM, amewahi kuwa Wazirikatika serikali ya Mapinduzi Zanzibar na pia Katibu wa NEC, Oganaizesheni.
 Mama Asha Abdallah Juma akipongezana na Mkurugenzi wa Mawsiliano na Umma, CCM, makao makuu, Daniel Chongolo, wakati wa mahafali hayo. Chongolo ametnukiwa shahada ya kwanza ya Mawasiliano ya Umma. Katikati ni pia ni Kada wa CCM, Rachel Kyala ambaye pia ametunukiwa shahada ya Mawasiliano ya umma. Picha zaidi BOFYA HAPA

MAKADA WA CCM WANG'ARA KATIKA MAHAFALI YA 25 YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA LEO

 Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT), Dk. Asha-Rose Migiro, akimpongeza Kada wa CCM, Asha Abdallah Juma, baada ya kumtunuku shahada ... [Read More]

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea Mweneyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipowasili Makao Makuu ya CCM, Jengo la White House, mjini Dodoma, kufunga mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, jana, Oktoba 24, Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.
 Mweneyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akionyesha kuwa mwenye furaha, alipowasili ukumbini kufunga mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, jana, Oktoba 24, 2013 mjini Dodoma. Mafunzo hayo yaliyokuwa ya siku nne yalifunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
 Ukumbi ukilipuka kwa mbinje, nderemo na vifijo, Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipowasili ukumbini, Makao Makuu ya CCM, mjini Dodoma kufunga mafunzo ya watendaji na viongozi wa CCM.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula, baada ya kuwasilini ukumbini na kulakiwa kwa shangwe na wahitimu wa mafunzo kwa wa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za mikoa na wilaya nchini mjini Dodoma, jana, Oktoba 24, 2013.
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akizungumza wakati wa kufunga mafunzo ya watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa hapa nchini, mjini Dodoma , jana , Oktoba 25, 2013. Kushoto ni Kinana na Kulia ni Mangula.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye (kulia) akizungumza namna mafunzo hayo yalivyoandaliwa na Idara yake ya Itikadi na Uenezi na kumalizika kwa mafanikio makubwa.
 Baadhi ya viongozi wa Jumuia na Sekretarieti wakiwa ukumbini
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa akitazama bango jipya la picha za wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, baada ya mabango hayo kugawiwa kwa washiriki wa mafunzo hayo ukumbini, wakati wa kufungwa mafunzo hayo. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai.
 Katibu wa NEC, Itikadi na uenezi Nape Nnauye akihamasisha baada ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kifunga mafunzo hayo.
 VYETI TUTAGAWA KAMA HIVI: Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akisema hivyo huku akimshika mkono mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Bashir Nkoromo, kabla ya kuanza kugawa vyeti kwa wahitimu wa mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM, ngazi za wilaya na mikoa, jana Oktoba 24, 2013, mjini Dodoma. Nkoromo ambaye ni Mpigapicha Mwandamizi wa Uhuru Publications Ltd, wachapishaji wa magazeti ya Uhuru,Mzalendo na Burudani,  ni Katibu Msaidizi katika Kitengo cha Mawasiliano na Umma, Idara ya Itikadi na Uenezi, CCM, Taifa.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi cheti Mwenyekiti wa Makatibu wa CCM wa mikoa, Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Steven Kazidi, alipofunga mafunzo ya utendaji bora kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa., jana, Oktoba, 24, Makao Makuu ya CCM mjini Dopdoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula na Watatu ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdultahman Kinana. Zaidi ya makatibu wa CCM wa mkoa wa wilaya zote nchini wamehitimu mafunzo hayo. Imetayarishwa na theNkoromo Blog

MWENYEKITI WA CCM, RAIS JAKAYA KIKWETE AFUNGA MAFUNZO KWA WATENDAJI WA CCM MJINI DODOMA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea Mweneyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipowasili Makao Makuu ya CCM, Jengo la White Hou... [Read More]

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akishuka kwenye ndege, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma jioni hii, kwa ajili ya kufunga semina ya mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa inayomalizika kesho.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimpokea Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete baada ya kuwasili mjini Dodoma
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akimsalimia Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Philip Mangula, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma jioni hii
 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye Uwanja wa Ndege mjini Dodoma baada ya kuwasili jioni hii.
 Katibu Mkuu wa CCM, Kinana akimwongoza Rais Kikwete kwenda eneo la mapumziko baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma, Adam Kimbisa
Mwenyekiti wa CCM, Rais Kikwete akiwasalimia wananchi waliofika kumlaki, Uwanja wa Ndege wa Dodoma jioni hii.

JK AWASILI MJINI DODOMA JIONI HII, KUFUNGA SEMINA YA WATENDAJI NA VIONGOZI WA CCM KESHO

 Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akishuka kwenye ndege, baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Dodoma jioni hii, kwa ajili ya kufunga s... [Read More]

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza mwanzini mwa siku ya tatu ya semina ya mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, katika ukumbi wa Sekretarieti, Jengo la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kushoto ni Katibu wa NEC, Oganaizesheni Mohamed Seif Khatib na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa mada kuhusu namna nzuri ya kuandaa mikutano, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Washiriki wa semina ya mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM, wakiwa wamefurika ukumbini katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Baadhi ya Wajumbe na Makatibu wa Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), wakiongozwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kusikiliza mada iliyokuwa ikitolewa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (hayupo pichani) katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akisalimiana na baadhi ya wajumbe, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu wa NEC, Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (kulia, safu ya mbele)akifuatilia kwa makini mada iliyokuwa ikitolewa na Nape (hayupo pichani), katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Katibu wa CCM, Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma, Kombo Kamote, akiongoza kuimba wimbo wa hamasa, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Kulia kwake ni Katibu wa CCM, wilaya ya Kigoma mjini, Augustine Minja.
 Baadhi ya wajumbe wakipitia ratiba, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Mkuu wa Mafunzo ya taaluma makao makuu ya CCM, Hadija Faraji (kushoto), akiwa miongoni mwa jopo la sekretarieti, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
 Baadhi ya wajumbe wakibadilishana mawazo, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma.
Sekretarieti ikiwa kazini, katika siku ya tatu ya semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa, leo Oktoba 23, 2013, Makao Makuu ya CCM mjini 
Dodoma. Imetayarishwa na theNkoromo Blog

SEMINA YA CCM KWA WATENDAJI NA VIONGOZI WAKE NGAZI ZA WILAYA NA MIKOA YAPAMBA MOTO LEO MJINI DODOMA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akizungumza mwanzini mwa siku ya tatu ya semina ya mafunzo kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za... [Read More]

KAMANDA MSTAAFU WA POLISI AFARIKI DUNIA LEO

[Read More]

Rais Kikwete
Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Ndugu Abdulrahaman Kinana kufuatia kifo cha ghafla cha Diwani wa Kata ya Njombe Mjini na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi kupitia Mkoa wa Njombe, Ndugu  Lupyana Fute.

Ndugu Fute alifariki ghafla tarehe 19 Oktoba, 2013 nyumbani kwake Mtaa wa Mgendela katika Kata ya Njombe Mjini kutokana na shinikizo la damu.

“Nimepokea kwa mshtuko na majonzi makubwa taarifa za kifo cha ghafla cha Diwani wa Kata ya Njombe Mjini na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama chetu, Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mheshimiwa Lupyana Fute ambaye, enzi za uhai wake, nilimfahamu kama Kiongozi Mchapakazi na Mwanachama Mwaminifu na Mwadilifu wa CCM aliyekisaidia sana Chama Cha Mapinduzi katika utekelezaji wa majukumu yake”, amesema kwa masikitiko Rais Kikwete katika Salamu zake za Rambirambi.  

Rais Kikwete amesema anaelewa fika kuwa kuondoka kwa ghafla kwa Mheshimiwa Fute kumeleta simanzi na majonzi makubwa siyo tu kwa Familia yake, bali pia kwa Wananchi aliokuwa akiwaongoza katika Wadhifa wake wa Udiwani, Wanachama wa Chama Cha Mapinduzi katika Mkoa wa Njombe, na kwa kweli kwa Wanachama wengine wa CCM kote nchini ambao wataukosa mchango wa Mwanachama huyu muhimu.

“Kutokana na Msiba huu Mkubwa, ninakutumia wewe Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahaman Kinana Salamu zangu za Rambirambi kwa kumpoteza mmoja wa Viongozi muhimu katika Chama chetu.  Vilevile kupitia kwako naomba Salamu zangu za Rambirambi na pole nyingi zifike kwa Familia ya Marehemu Lupyana Fute kwa kumpoteza Kiongozi na Mhimili Madhubuti wa Familia”, amesema Rais Kikwete na kuongeza,

“Ninawahakikishia kuwa niko pamoja nao katika kipindi hiki kigumu cha Maombolezo ya Mpendwa wao, na namuomba Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema aipokee na kuilaza Mahala Pema Peponi Roho ya Marehemu Lupyana Fute, Amina”.

Vilevile Rais Kikwete amemuomba Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahaman Kinana kumfikishia Salamu zake za Rambirambi kwa Wana-CCM kote nchini hususan wa Mkoa Mpya wa Njombe ambao  Marehemu alikuwa akiwawakilisha katika Wadhifa wake wa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM.  Amewaomba wafuate mfano mzuri wa uchapakazi, uaminifu na uadilifu wa Marehemu katika utendaji wa kazi zao.      

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
22 Oktoba, 2013


JK AMLILIA DIWANI KATA YA NJOMBEA MAREHEMU LUPYANA

Rais Kikwete Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete amemtumia Salamu za Rambirambi Katibu Mku... [Read More]


 Semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa nchini kote, ambavyo ilianza jana mjini Dodoma kwa kufunguliwa na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, leo imeendelea kupamba moto kwa mada mbalimbali, katika ukumbi wa sekreterieti ndani ya Jumba la White House, Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma. Pichani, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akitoa maneno ya utangulizi kabla ya mada kuanza kutolewa. Wengine kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba, Katibu wa NEC, Uchumi na Fedha, Zakiah Meghji na Katibu wa NEC, Itukadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Washiriki wakiwa kwenye semina hiyo leo asubuhi
 Washiriki wakifuatilia mada kwenye semina hiyo asubuhi hii
 Washiriki wakifuatilia mada
 Washiriki wakifurahia mada motomoto
 Washiriki kutoka Dar es Salaam, wakifuatilia kwa makini mada (kushoto) ni Katibu wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Abilah Mihewa
 Nape akitoa angalizo kuboresha usikivu wa mada kwenye semina hiyo
Maofisa wa Chama kutoka Makao Makuu ya CCM wakiwa kwenye semina hiyo. (wacheki pande za kulia)

SEMINA YA MAFUNZO KWA WATENDAJI NA VIONGOZI WA CCM NGAZI ZA WILAYA NA MIKOA YAENDELEA LEO MJINI DODOMA

 Semina ya mafunzo ya siku nne kwa watendaji na viongozi wa CCM ngazi za wilaya na mikoa nchini kote, ambavyo ilianza jana mjini Dodoma kwa ... [Read More]