Google PlusRSS FeedEmail
Bandari ya Zanzibar
 Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu ya UVCCM ambao wamechanganyika na abiria wengine, wakiwa kwenye gati baada ya kushuka katika boti jioni hii
 Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu la UVCCM kutoa Tanzania Bara wakitoka bandarini baada ya kuwasili mjini Zanzibar kwa ajili ya kikao cha Baraza hilo kitakachofanyika kesho, Afisi Kuu ya CCM, Kisiwandui
 Baadhi yao wakisubiriana kabla ya kupanda mabasi maalum yaliyoletwa bandarini kuwabeba
 Wajumbe wakiwa katika mabasi
 Wajumbe wakiwasili Afisi Kuu ya UVCCM Zanzibar
 Baada ya wajumbe hao kushuka

Kikundi cga Bras Band cha UVCCM Zanzibar kikijifua kwa mazoezi kwa ajili ya mkutano wa kesho.Imetayarishwa na theNkoromo Blog

WAJUMBE BARAZA KUU UVCCM KUTOKA TANZANIA BARA WAWASILI ZANZIBAR JIONI HII

Bandari ya Zanzibar  Baadhi ya wajumbe wa Baraza Kuu ya UVCCM ambao wamechanganyika na abiria wengine, wakiwa kwenye gati baada ya kushuka k... [Read More]

 Baadhi ya wajumbe wakiwa Makao Makuu ya UVCCM, jijini Dar es Salaam, tayari kwa safari ya kwenda Zanzibar kwenye kikao cha Baraza Kuu ya Jumuia hiyo, kitakachofanyika kesho.
 Wajumbe wakiwa nje za jengo la Umoja wa Vijana wa CCM, mjini Dar es Salaam, kabla ya kuanza safari yao kwenda Zanzibar
 Baadhi ya wajumbe wakiwa Ofisi za UVCCM mjiniu Dar es Salaam, kabla ya kuondoka kwenda Zanzibar kwenye kikao hicho.
 Wajumbe wakiwa kwenye ofisi ya UVCCM makao makuu
Baadhi ya wajumbe wakipanda mabasi kutoka makao makuu ya UVCCM kwenda Bandarini kubanda boti kwenda Zanzibar kwenye kikao hicho cha Baraza Kuu la UVCCM leo
Baadhi ya wajumbe wakiwa bandari ya Dar es Salaam, kupanda boti
Wajumbe wakiwa kwenye boti mjini Dar es Salaam, tayari kwa safari ya Zanzibar
Wajumbe wakiwa kwenye boti yatari kwa safari ya Zanzibar. Imetayarishwa na theNkoromo Blog

WAJUMBE WA BARA WAENDA ZANZIBAR KWENYE BARAZA KUU LA UVCCM TAIFA

 Baadhi ya wajumbe wakiwa Makao Makuu ya UVCCM, jijini Dar es Salaam, tayari kwa safari ya kwenda Zanzibar kwenye kikao cha Baraza Kuu ya Ju... [Read More]

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Gelorious Luoga (kulia) akibadilishana mawazo na Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Rojas Romuli (kushoto) na Katibu Msaidizi Mkuu, Idara ya Itikadi na Uenezi Makao Mkuu, Anamringi Macha, walipokutana leo asubuhi nje ya Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba jijini Dar es Salaam. Luoga na Romuli wameteuliwa kushinka nafasi hizo katika vikao vya Kamati Kuu na NEC vilivyofanyika mjini Dodoma, hivi karibuni

VIONGOZI WA CHAMA WANAPOKUTANA

Naibu Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi Tanzania Gelorious Luoga (kulia) akibadilishana mawazo na Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Rojas Romuli ... [Read More]

 Baadhi ya wawakilishi wa Mtandao wa Wazee wakiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye nje ya ofisi za Makao Makuu ya Chama Dodoma leo tarehe 30 Agosti 2013.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na mmoja wa wawakilishi wa Mtandao wa Wazee Bibi Koku , Wazee hao walifika Makao Makuu ya CCM kuja kuzungumza madai ya Pensheni zao ambayo waliahidiwa na serikali.

CCM KUWASAIDIA WAZEE

 Baadhi ya wawakilishi wa Mtandao wa Wazee wakiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye nje ya ofi... [Read More]

IGP SAIDI MWEMA APANGUA MAKAMNADA

IGP SAID MWEMA   DAR ES SALAAM, Tanzania Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa Mikoa... [Read More]



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

KUREJESHWA KWA URUSHAJI MATANGAZO RADIO IMAAN FM NA KWA NEEMA FM RADIO

1.0 Utangulizi:

Mnamo tarehe 26/02/2013 Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ilitoa uamuzi wa kuvifungia vituo vya utangazaji vya Radio Imaan ya mjini Morogoro na Kwa Neema FM Radio ya jijini Mwanza baada ya kukiuka Sheria na Kanuni za Utangazaji.

Kamati ya Maudhui iliuita uongozi wa vituo hivyo tarehe 11/02/2013 na tarehe 14/02/2013 ili kujitetea na vyote vilikiri kosa. Baada ya kutafakari utetezi wa Radio Imaan na Radio ya Kwa Neema FM na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Utangazaji, Kamati iliamua kutoa adhabu kwa vituo vyote viliwi kama ifuatavyo:-

a)   Vituo vyote vilipewa  onyo pamoja na kufungiwa kurusha matangazo kwa kipindi cha miezi sita kuanzia tarehe 26/02/2013;

b)  Vituo vyote vilitakiwa kuithibitishia Mamlaka ya Mawasiliano na Kamati ya Maudhui kwa maandishi kuwa hawatarejea kutenda kosa la aina hiyo au linalofanana na hilo. Ikiwa vitarudia Kamati ya Maudhui haitasita kuvifutia leseni zao za utangazaji.

2.0 Kutekeleza adhabu na hatua zilizochukuliwa na vituo hivyo
      na Mamlaka ya Mawasiliano:   

Baada ya Uamuzi huo kusomwa, vituo vyote viwili vilianza kutekeleza adhabu mara moja kama ilivyotakiwa kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utangazaji. Mamlaka ya Mawasiliano ilipokea barua ya udhibitisho wa kutofanya kosa tena yaani “Commitment letter” pamoja na sera ya uhariri (Editorial Policy) na ratiba ya vipindi kutoka kwa vituo vyote viwili.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ilifanya ukaguzi kwa vituo vyote viwili ili kujiridhisha na kuzipitia sera za uhariri pamoja na mwongozo wa vipindi kabla ya kuvifungulia.

3.0 Kurejeshwa kwa Matangazo

Kamati ya Maudhui iliandika barua tarehe 27/08/2013 kuhusu kuvifungulia vituo hivyo vya utangazaji vya Radio Imaan ya mjini Morogoro na Kwa Neema FM Radio ya jijini Mwanza baada ya kutumikia adhabu kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Utangazaji. Vituo hivi vimeanza kurusha matangazo yake kuanzia leo tarehe 28/08/2013 baada ya muda wa adhabu kuisha.

Kamati ya Maudhui inapenda kutumia fursa hii kuvionya vyombo vya habari vya utangazaji vya redio na televisheni kuwa makini katika kutekeleza masharti ya leseni pamoja na kufuata Sheria na Kanuni za Utangazaji. Kamati ya Maudhui haitasita kutoa adhabu kali au kuvifungia vituo vitakavyokiuka Masharti ya leseni, Sheria pamoja na Kanuni za Utangazaji au hata kuvifutia leseni zao.

Kamati ya Maudhui inatoa wito kwa vyombo vya habari vya utangazaji kuzingatia Sheria, Kanuni na Masharti ya leseni ilikuboresha Sekta ya Utangazaji na kudumisha amani nchini.



Eng. Margaret Munyagi
Mwenyekiti,
Kamati ya Maudhui Ya TCRA,
S.L.P. 474,
DAR ES SALAAM.
28/08/2013

KUREJESHWA KWA URUSHAJI MATANGAZO RADIO IMAAN FM NA KWA NEEMA FM RADIO

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUREJESHWA KWA URUSHAJI MATANGAZO RADIO IMAAN... [Read More]

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, wakati akiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo, Agosti 29, 2013 baada ya kumaliza mapumziko yake ya siku tatu nchini. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsindikiza Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, wakati akiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo, Agosti 29, 2013 baada ya kumaliza mapumziko yake ya siku tatu nchini. Picha na OMR

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsindikiza Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, wakati akiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo, Agosti 29, 2013 baada ya kumaliza mapumziko yake ya siku tatu nchini. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimsindikiza Rais wa Burundi, Pierre Nkurunzinza, wakati akiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo, Agosti 29, 2013 baada ya kumaliza mapumziko yake ya siku tatu nchini. Picha na OMR Rais wa Burundi, Piere Nkurunzinza, akiagana na baadhi ya maofisa wa Ofisi ya Makamu wa Rais, waliofika uwanjani hapo kumsindikiza leo Agosti 29, baada ya Rais huyo kumaliza mapumziko yake ya siku tatu nchini. Kushoto ni Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal. Picha na OMR
IMETAYARISHWA NA BASHIR NKOROMO

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AAGANA NA RAIS WA BURUNDI NKURUNZINZA BAADA YA KUMALIZA MAPUMZIKO YAKE NCHINI

  Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na Rais wa Burundi, Pierre  Nkurunzinza, wakati ak... [Read More]

Viongozi wa Mbio za mwenge wakiwa na wananchi wa wilaya ya morogoro mjini wakati wa makabidhiano ya mwenge wa uhuru leo wakati mwenge huo ulipomaliza mbio zake wilaya ya Morogoro mjini na kukabidhiwa wilaya ya Morogoro vijijini
Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mh Said Amanzi akiwa Na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro Jorvis Simbeye  wakati wa mbio za mwenge
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro Jorvis Simbeye akikabidhi Mwenge wa uhuru kwa mkurugenzi wa wilaya ya Morogoro vijijini leo
Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro Jorvis Simbeye akimkabidhi  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Morogoro Vijijini, Julis Madiga  Mwenge wa Uhuru leo.
Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mh Said Amanzi akiwa na Mwenge wa Uhuru mara baada ya kukabidhiwa leo.
Wabunge wa majimbo ya Morogoro vijijini  Mh Innocent kalogeris wa Jimbo la Morogoro kusini akiwa na Dk Lucy Nkya wa jimbo la Morogoro kusini mashariki leo wakati wa makabidhiano ya Mwenge wa Uhuru

MWENGE WA UHURU WAENDELEA NA MBIO ZAKE MOROGORO

Viongozi wa Mbio za mwenge wakiwa na wananchi wa wilaya ya morogoro mjini wakati wa makabidhiano ya mwenge wa uhuru leo wakati mwenge huo ul... [Read More]

 Msaidizi wa Makamu wa Rais wa masuala ya Maendeleo ya Jamii, Mgeni Feruzi Kayanda, akimkabidhi Pikipiki Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Geodan Rugimbana, aliyeikabidhi Pikipiki hiyo kwa wananchi wa Mji mpya wa Mabwe pande kwa niaba ya Makamu wa Rais, wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo katika mji huo mpya. Kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mji Mpya wa Mabwe Pande, Abdallah Kunja. Picha na OMR

 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Geodan Rugimbana, akimkabidhi Pikipiki na nyaraka muhimu, Mwenyekiti wa Kamati ya Mji Mpya wa Mabwe Pande, Abdallah Kunja, wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo katika mji huo mpya, ambapo Mkuu wa Wilaya, alikabidhi Pikipiki hiyo kwa wananchi wa Mji mpya wa Mabwe pande kwa niaba ya Makamu wa Rais. Picha na OMR

 Sehemu ya wakazi wa Mji Mpya wa Mabwe Pande waliohudhuria hafla hiyo ya makabidhiano.

Msaidizi wa Makamu wa Rais wa masuala ya Maendeleo ya Jamii, Mgeni Feruzi Kayanda, akizungumza machache wakati wa hafla hiyo baada ya makabidhiano.Picha na OMR

MAKAMU WA RAIS DKT BILAL ATOA MSAADA WA PIKIPIKI KWA WATENDAJI WA KAMATI YA MJI MPYA WA MABWE PANDE

 Msaidizi wa Makamu wa Rais wa masuala ya Maendeleo ya Jamii, Mgeni Feruzi Kayanda, akimkabidhi Pikipiki Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Geodan... [Read More]

DODOMA,Tanzania
Pamoja na kubatilisha uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Kagera wa kuwafukuza  madiwani wanane wa CCM katika Halimashauri ya Bukoba mjini kwa utovu wa nidhamu, leo Kamati Kuu ya CCM imeagiza serikali kumtuma Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kufanya ukaguzi maalumu katika Halmashauri hiyo kupata ukweli halisi wa tuhuma za ufisadi anaodaiwa kufanya Meya wa Halmashauri hiyo, Anatory Amani.

Meya  Anatory Amani
Kamati Kuu imechukua hatua hiyo, baada ya kuwahoji Mwenyekiti na Katibu wa CCM mkoa wa Kagera, Mwenyekiti na Katibu wa CCM wilaya ya Bukoba mjini na Mbunge wa Bukoba mjini Hamisi Kagasheki na Meya wa Halmashauri hiyoi, mjini Dodima  na kubaini kwamba moja ya mambo yanayodaiwa kuchangia sakata hilo hadi kufukuzwa madiwani hao, ni kuwepo kwa tuhuma za ufisadi dhidi ya Meya huyo katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza leo na mjini hapa, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye amesema, leo Kamati Kuu imetoa uamuzi wa kubatilisha hatua ya kufukuzwa kwa madiwani hao, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15), ambayo inaelekeza kazi na majukumu ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa.

“Ibara hiyo inasema kumwachisha au kumfukuza uongozi, kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo” alisema Nape.

Kufuatia hatua hiyo, CCM imewataka madiwani hao kuendelea na kazi zao na  imewaonya viongozi wote wa chama mkoa, wilaya, Meya na mbunge kuhakikisha inarudisha hali ya utulivu na amani.

Nape alisema Kamati Kuu imewaonya madiwani wa CCM wa Manispaa ya Bukoba, Mbunge wa Bukoba Mjini na Meya kwa kusababisha kukosekana kwa utulivu, mshikamano na amani katika Manispaa na Chama.

“Wakati tuhuma za Meya zikichunguzwa, Kamati Kuu inawataka madiwani wa CCM  kurejesha utulivu kwenye manispaa na Chama kwa ujumla ili kufanikisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwaletea maendeleo wananchi wa Bukoba,’’alisema.

Madiwani waliokuwa wamevuliwa na uanachama katika sakata hilo ni Richard Gaspar (Miembeni), Murungi Kichwabuta (Viti Maalumu), Alexander Ngalinda ambaye pia ni Naibu Meya (Buhembe), Yusuf Ngaiza ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Wilaya (Kashai), Deusdedit Mutakyahwa (Nyanga), Robert Katunzi (Hamugembe), Samwel Ruhangisa (Kitendaguro) na Dauda Karumuna (Ijuganyondo).

Inadaiwa madiwani hao waliungana na wenzao wa wapinzani kupinga maamuzi mbalimbali yaliyofanya na Meya Tarimo, madiwani hao ni Dismas Rutagwelera (Rwamishenyi), Israel Mlaki (Kibeta), Winifrida Mkono (Viti Maalumu), Conchesta Rwamlaza ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu CHADEMA na Ibrahim Mabruk (Bilele), Felician Bigambo (Bakoba) na Rabia Badru (Viti Maalumu - CUF).

Maamuzi yaliyofanywa na Meya huyo, ambayo yamepingwa na madiwani kuwa ameiingiza manispaa katika ufisadi kwenye miradi kadhaa. Miradi hiyo ni upimaji wa viwanja 5,000 unaodaiwa mkopo wake wa sh. bilioni 2.9 kutoka Mfuko wa Dhamana ya Uwekezaji (UTT) haukufuata taratibu, na wananchi hawakushirikishwa ipasavyo.

Tuhuma nyingine ni mradi wa ujenzi wa soko. Meya anadaiwa kusitisha malipo ya ushuru na kutaka kuwaondoa wafanyabiashara bila kufuata utaratibu pamoja na kudaiwa kukopa sh. milioni 200 katika Benki ya Uwekezaji (TIB) bila kibali cha Baraza la Madiwani.

Aidha, inadaiwa kuwa Meya huyo alitoa taarifa katika kikao cha baraza hilo kuwa TIB iliwapa ruzuku ya sh milioni 90, lakini hakueleza misingi yake, pamoja na kuwepo kwa mradi wa kuosha magari ambao unadaiwa kutumia kiasi cha sh. milioni 297 zinazotiliwa shaka.

Pia, Meya ameshindwa kutoa mchanganuo wa mapato na matumizi ya mradi kiasi cha sh. milioni 134, za ujenzi wa kituo cha mabasi. Imetayarishwa na theNkoromo Blog.
************************************TAARIFA RASMI YA CCM
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.
 
Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

 
Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15). Ibara hiyo inasomeka kuwa moja ya kazi ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa ni:-


“Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo”.

 
Aidha, Kamati Kuu imewaonya Madiwani wa CCM wa Manispaa ya Bukoba, Mbunge wa Bukoba Mjini na Meya kwa kusababisha kukosekana kwa utulivu, mshikamano na amani katika Manispaa na Chama.
 
Kamati Kuu pia imeitaka Serikali kumwagiza mdhibiti na mkaguzi mkuu wa serikali(CAG) kufanya ukaguzi maalum wa haraka wa mambo yanayolalamikiwa dhidi ya Meya ili ukweli ujulikane na matokeo ya uchunguzi huo yasilishwe kwenye baraza la madiwani ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria na taratibu zinazoongoza Serikali za Mitaa.
 


Wakati tuhuma hizo dhidi ya Meya zikichunguzwa; Kamati Kuu inawataka Madiwani wa CCM  kurejesha utulivu kwenye Manispaa na Chama kwa ujumla ili kufanikisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwaletea maendeleo wananchi wa Bukoba. 
Imetolewa na:-
 
Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM
ITIKADI NA UENEZI
27/08/2013

KAMATI KUU YA CCM YATENGUA KUFUKUZWA UANACHAMA MADIWANI WANANE HALMASHAURI YA BUKOBA , YAMWAGIZA CAG KUFANYA UKAGUZI MAALUM KATIKA HALMASHAURI HIYO KWA HATUA STAHIKI

DODOMA,Tanzania Pamoja na kubatilisha uamuzi wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Kagera wa kuwafukuza  madiwani wanane wa CCM katika Halimasha... [Read More]

 Mwenyekiti wa Mkoa wa Kagera Constansia Buhiye akizungumza na aliyekuwa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Hamis Suleiman Dadi nje ya ukumbi wa NEC, Dodoma leo, kushoto ni Katibu wa Mkoa wa Kagera Avelin Mushi.

 Meya wa Bukoba ndugu Anatory Amani akizungumza na Mwneyekiti wa UVCCM nje ya ukumbi wa NEC mara tu baada ya kutoka kwenye mahojiano na kamati kuu ya CCM.
Watumishi wa Makao Makuu CCM, kutoka kushoto ni Suleiman Serera,Adam Soud, Katibu Mpya wa  CCM Mkoa wa Morogoro ndugu Romuli  John na Annamringi Macha wakibalishana mawazo nje ya ukumbi wa NEC ,Dodoma.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari juu ya uamuzi wa kamati kuu kubatilisha uamuzi wa kufukuzwa madiwani wa Bukoba.

MATUKIO MBALI MBALI NJE YA UKUMBI WA NEC

  Mwenyekiti wa Mkoa wa Kagera Constansia Buhiye akizungumza na aliyekuwa Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Hamis Suleiman Dadi nje ya ukumbi wa N... [Read More]



 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi  wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wa kamati kuu wa kubatilisha kufukuzwa kwa madiwani wa Bukoba nje ya ukumbi wa NEC.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa imejadili na kutolea maamuzi pamoja na mambo mengine suala la Madiwani wanane waliotangazwa kufukuzwa uanachama na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera.

Katika maamuzi yake, Kamati Kuu imebatilisha uamuzi uliofanywa na Halmashauri Kuu CCM ya Mkoa wa Kagera Agosti 13, 2013 wa kuwafukuza uanachama Madiwani hao. Hivyo Madiwani hao wanane ni wanachama halali wa CCM.

Kamati Kuu imetoa uamuzi huo, baada ya kubaini kuwa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera haikuzingatia Katiba ya CCM ya 1977 Toleo la 2012 Ibara ya 93 (15). Ibara hiyo inasomeka kuwa moja ya kazi ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa ni:-
“Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri Kuu ya CCM ya Mkoa, isipokuwa kwa suala la kumvua uanachama au uongozi Diwani lisifanyike hadi Kamati Kuu imearifiwa na kutoa maelekezo”.

Aidha, Kamati Kuu imewaonya Madiwani wa CCM wa Manispaa ya Bukoba, Mbunge wa Bukoba Mjini na Meya kwa kusababisha kukosekana kwa utulivu, mshikamano na amani katika Manispaa na Chama.

Kamati Kuu pia imeitaka Serikali kumwagiza mdhibiti na mkaguzi mkuu wa serikali(CAG) kufanya ukaguzi maalum wa haraka wa mambo yanayolalamikiwa dhidi ya Meya ili ukweli ujulikane na matokeo ya uchunguzi huo yasilishwe kwenye baraza la madiwani ili hatua stahiki zichukuliwe kwa mujibu wa sheria na taratibu zinazoongoza Serikali za Mitaa.

Wakati tuhuma hizo dhidi ya Meya zikichunguzwa; Kamati Kuu inawataka Madiwani wa CCM  kurejesha utulivu kwenye Manispaa na Chama kwa ujumla ili kufanikisha utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuwaletea maendeleo wananchi wa Bukoba.

Imetolewa na:-

Nape Moses Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM
ITIKADI NA UENEZI
27/08/2013

KAMATI KUU CCM YABATILISHA UAMUZI WA HALMASHAURI KUU YA CCM BUKOBA

  Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi  wa CCM, Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uamuzi wa kamati kuu wa kubatilisha kufukuz... [Read More]

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Jaji Francis Mutungi na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Mhe John Tendwa baada ya kumuapisha Jaji Mutungi Ikulu jijini Dar es Salaam .

RAIS KIKWETE NA MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA MPYA JAJI FRANCIS MUTUNGI NA MSTAAFU MHE JOHN TENDWA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Jaji Francis Mutungi na Msajili wa Vyama vya Siasa Mstaafu Mhe John T... [Read More]

MAKATIBU WA CCM WA WILAYA WALIOTEULIWA NA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA TAIFA TAREHE 23/08/2013

1.            Ndugu Ashura Amanzi 2.            Ndugu Rukia Saidi Mkindu 3.            Ndugu Elias J. Mpanda 4.            Ndugu Jonathan M... [Read More]