Google PlusRSS FeedEmail
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wakazi wa Dar es Salaam kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Mwembeyanga.
 Wananchi waliohudhuria mkutano huo, uliofanyika juzi,  kumpongeza Rais
Jakaya Kikwete kwa hotuba yake aliyoitoa wakati wa kuzindua Bunge Maalum la
katiba,linaloendelea mjini Dodoma.


 Kinana akionyesha kadi ya Chadema aliyokabidhiwa na Ramadhan (kushoto).
 Wananchi wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe maalumu.

 Balozi Ali Abeid Karume, akizungumza katika mkutano huo

 Mwenyekiti wa Chama cha SDF cha Cameroun, John Frundi, akizungumza katika
mkutano huo. Kushoto ni Kinana na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es
Salaam, Ramadhan Madabida.

 WANACHAMA wa CCM, wakimpongeza Kinana kutokana na juhudi zake katika
kusimamia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Baadhi ya wajumbe waalikwa waliohudhuria mkutano huo.


Picha zote na Khamis Hama

MKUTANO WA KINANA MWEMBEYANGA WAWEKA HISTORIA

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia maelfu ya wakazi wa Dar es Salaam kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwa... [Read More]

KINANA AZURU KATA ZA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA LEO KATIKA ZIARA YAKE WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Mar 31, 2014
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Rukwa,  Hypolitus Matete (aliyenyoosha mkono), akimuonyesha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana mandahari ya eneo la Ziwa Tanganyika, linalotumiwa na wavuvi katika eneo la Kabwe wilayani Nkasi mkoani humo, Kinana alipokuwa katika ziara ya kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM na kusikiliza kero za wananchi na kujadili nao njia ya kuzitatua katika eneo hilo la Wavuvi, leo.
Katibu Mkuu wa CCM akitazama eneo la uvuvi katika ziawa Tanganyika, kwenye eneo la Kabwe mkoani Rukwa leo

Mfanyabiashara ya kusafirisha na kusindika samaki kutoka ziwa Tanganyika, Mohamed Shibibi (wapili kushoto) akimpatia maelezo  Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana jinsi anavyohifadhi samaki katika majokofu baada ya kuvuliwa, Kinana alipokagua shughuli za mfanyabiashara huyo, kwenye eneo la wavuvi wa Kata ya Kabwe, wilayani Kansi mkoani Rukwa leo. Kushoto ni Mjumbe wa NEC, Balozi Ali Karume.
Mfanyabiashara ya samaki Abuu Kitandu, akimuonyesha Kinana ukaushaji wa samaki kwenye kituo cha wavuvi cha Kabwe, wilayani Nkasi mkoani Rukwa
Kinana akitazama lundo la samaki aina ya migebuka kwenye kituo cha wavuvi cha Kabwe, katika ziwa Tanganyika
Mkazi wa Kabwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa akiwa na mzigo wa migebuka aliowanunua kwa wavuvi katika ziwa Tanganyika
Mtoto Khalifa Saidi (5) akiwa amebeba samaki kwenye eneo la wavuvi la Kabwe, wilayani Nkasi
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wajengo la Ofisi ya CCM Kata ya Kabwe, mkoani Rukwa, leo.
Wananchi wa Kabwe, wakiwa wamebeba samaki mkubwa kutoka Ziwa Tanganyika, wakati Kinana na Mbunge wa Nkasi Kaskazini Ali Kessy wakiwafuata kwa nyumba baada ya kutoka kukagua shughuli za wavuvi katika eneo lawafugaji la Kabwe mkoani Rukwa. 
Boti za wavuvi zikitia nanga ufukweni eneo la Kabwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akihutubia mamia ya wananchi kwenye Ofisi ya CCM Kata ya Kabwe, wilayani Nkasi mkoani Rukwa leo.
Mjumbe wa NEC, Balozi Ali Karume, akihutubia wananchi katika mkutano wa Kinana, uliofanyika leo kwenye Ofisi ya CCM Kata ya Kabwe leo.
Wananchi wa Kata ya Kabwe wakimshangilia Kinana
Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma Makao Makuu ya CCM, Godfrey Chongolo, akiwa na kina mama waliokuwa wakikunja samaki aina ya migebuka katika mwambao wa ziwa Tanganyika eneo la Kabwe, Wilayani Nkasi mkoani Rukwa. (Picha zote na Bashir Nkoromo wa CCM Blog)

KINANA AZURU KATA ZA MWAMBAO WA ZIWA TANGANYIKA LEO KATIKA ZIARA YAKE WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA Mar 31, 2014  Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Ru... [Read More]


DSC_0154
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh akiteta jambo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya uzinduzi wa toleo jipya la gari aina ya Mercedes Benz E-Class uliofanyika jijini Dar kwenye hoteli ya Capetown Fish Market.
DSC_0191
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh (wa pili kulia) na Meneja Masoko wa CFAO Motors, Bi. Tharaia Ahmed (wa pili kushoto) wakibadilishana mawazo na wageni waalikwa waliohudhuria kwenye uzinduzi wa toleo jipya la Mercedes Benz E-Class uliofanyika kwenye hoteli ya Capetown Fish Market jijini Dar.(Picha na Zainul mzige)
.Ni E-Class inaweza kutembea bila dereva
.Pia inafaa kwa matumizi yoyote na imara
Na Damas Makangale, MOblog Tanzania
KAMPUNI ya CFAO Motors Tanzania hivi karibuni wamezindua gari mpya aina ya Mercedes-Benz E-Class Saloon na Estate yenye muonekano bora zaidi na inaweza kutembea bila dereva amesema Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo.
Akizungumza na wageni waalikwa jijini Dar es Salaam katika uzinduzi rasmi wa gari hilo la Meredes-Benz, E-Class, Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors Tanzania, Wayne McIntosh amesema gari hiyo nia aina mpya kabisa na kisasa zaidi kutengenezwa na kampuni hiyo.
“wakati wa majaribio nchini Ujerumani gari hii iliweza kutembea kilometa kadhaa bila kuwa na dereva kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu kabisa,” amesema McIntosh.
DSC_0218
Wanenguaji wa kizungu wa Maendeleo Dance Group wakiburudisha tukio hilo la uzinduzi wa toleo jipya la Mercedes Benz E-Class jijini Dar es Salaam.
Amesema gari hiyo imetengezwa kwa ubunifu na teknolojia ya hali ya juu kabisa na wataalamu na mainjia kutoka nchini Ujerumani wenye uzoefu na utalaamu wa juu duniani.
McIntosh alisisitiza kwamba gari hiyo inaweza kabisa kutumiwa na mtu yoyote hapa duniani kutokana na muundo wake na teknolojia iliyotumika ni ya kisasa kabisa kumwezesha dereva au mtumiaji kuwa katika hali ya utulivu wakati wote wa safari.
“gari hii ni ya kimataifa yenye uwezo wa kumudu aina yeyote ya misukosuko barabarani na ni salama kwa mtumiaji wakati wote,” aliongeza.
DSC_0284
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors Tanzania, Wayne McIntosh akizungumza na wageni waalikwa katika uzinduzi wa gari hiyo mpya katika soko la Tanzania kwenye hoteli ya Cape Town Fish Market Msasani jijini Dar es Salaam.
DSC_0237
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Wayne McIntosh, akizindua rasmi Mercedez Benz aina ya E-Class jijini Dar esSalaam kwenye hafla fupi iliyofanyika kwenye hoteli ya Capetown Fish Market.
DSC_0232
Sasa imezinduliwa rasmi katika soko la Tanzania.
DSC_0239
Toleo jipya la gari aina ya Mercedes Benz E-Class lililozinduliwa rasmi jijini Dar es Salaam na kampuni ya CFAO Motors.
DSC_0257
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia tukio hilo la kipekee.
DSC_0262
DSC_0294
Mmoja wa wageni waalikwa akionekana kuvutiwa na toleo jipya la Mercedes Benz E-Class.
DSC_0418
DSC_0296
Mwakilishi wa TV 1 kutoka nchini Ghana akipozi na gari matata aina ya Mercedes Benz E-Class kwenye hafla fupi ya uzinduzi uliofanyika mwishoni mwa juma jijini Dar.
DSC_0304
Muonekano wa ndani wa gari hilo lenye speed 260.
DSC_0369
DSC_0373
Mmoja wa models aliyepamba uzinduzi huo akipozi kwenye toleo jipya la Mercedes Benz E-Class.
DSC_0380
Muonekano wa nyuma.
DSC_0430
Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Wanawake Tanzania, Bi.Margareth Chacha akifanyiwa mahojiano na TV1 ambapo akielezea mapenzi yake na magari ya aina ya Mercedes Benz ambapo hapo awali alikuwa akitumia na panapomajaliwa ya Mungu siku moja atamiliki toleo jipya la Mercedes Benz E-Class.
DSC_0414
Meneja Masoko wa Kampuni ya CFAO Motors, Tharaia Ahmed akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Wanawake Tanzania, Bi.Margareth Chacha kwenye hafla hiyo. Katikati ni Hellen Kiwia kutoka Frontline Management.
DSC_0321
Meneja Masoko wa CFAO Motors, Bi. Tharaia Ahmed akifafanua jambo kwa mmoja wa wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa toleo jipya la Mercedes Benz E-Class.
DSC_0355
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Wayne McIntosh, akisalimiana na mmoja wa wageni waalikwa Mkurugenzi Mkuu wa benki ya Wanawake Tanzania, Bi.Margareth Chacha (kushoto) kwenye hafla hiyo fupi ya uzinduzi wa toleo jipya la Mercedes Benz E-Class. Katikati ni Tender Manager wa CFAO Motors Bw. Marco Kahabi.
DSC_0197
Crew ya stesheni mpya ya TV 1 nao waliokuwa ni miongoni mwa wageni waalikwa.
DSC_0200
 

CFAO MOTORS WAZINDUA TOLEO JIPYA LA MERCEDES BENZ JIJINI DAR

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya CFAO Motors, Bw.Wayne McIntosh akiteta jambo na baadhi ya wageni waalikwa kwenye hafla fupi ya uzinduzi w... [Read More]


DSC_0271

Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe akisaini kitabu cha wageni cha Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious kwenye sherehe za uzinduzi wa Umoja huo zilizofanyika mwishoni mwa juma kwenye Hoteli ya Ocean View Beach Resort mjini Unguja.(Picha zote na Zainul Mzige).

Na. Zainul Mzige, Zanzibar.

UMOJA wa Wanawake wa Zanzibarlicious umeamua kuwakomboa wanawake kutoka katika utumwa wa kiuchumi kwa kuwawezesha kwa kuwapa ujuzi na maarifa ili kujikwamua kwenye umasikini.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa umoja huo, Umul-kulthum Ansel wakati wa uzinduzi wa umoja huo kwenye sherehe zilizofanyika mwishoni mwa juma katika Hoteli ya Ocean View Beach Resort mjini Unguja.

Alisema lengo la kuwakwamua wanawake ni kutokana na kuonekana wao na watoto ni waathirika wakuu wa mabadiliko ya kiuchumi na kisiasa yanayoendelea katika maeneo mbalimbali ulimwenguni hasa katika bara la Afrika.

“Umoja huu umeundwa kwa lengo la kuwashajihisha,kuwahamasisha ,kuwaunganisha na kuwaendeleza wanawake kwa kuwapa ujuzi na maarifa ili waweze kujitambua na kuithamini nafasi yao katika kuleta maendeleo,”alisema.

DSC_0284

Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious Bi. Evelyne Wilson (wa pili kushoto) akitoa maelezo ya picha na kazi mbalimbali walizofanya kwa jamii mara baada ya kuwasili mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious, Bi. Umul-Kulthum Ansel (Madam Ummy).

Alisema malengo ya umoja huo ulioanzishwa mwaka 2011 na kusajiliwa mwaka jana ni kumuendeleza na kumuwezesha mwanamke kiuchumi,kijamii na kimwenendo.

Alisema umoja huo umekuwa ukitoa elimu ya ujasiriamali kwa vikundi vya wanawake na kuwawezesha kubuni biashara ndogondogo na jinsi ya kuweza kutafuta mitaji kutoka taasisi mbalimbali za kitaifa.

“Pia tunatoa ushauri nasaha kwa masuala ya familia, waathirika wa virusi vya Ukimwi na Dawa za Kulevya,”alieleza Mwenyekiti huyo.

DSC_0289

Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe akitizama picha mbalimbali zinazoonyesha kazi walizofanya Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious kwa jamii inayowazunguka visiwani humo.

Vilevile Zanzibaliciuos inatoa ushauri wa kisheria katika masuala ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto pamoja na kuwakutanisha wanawake kutoka sehemu mbalimbali kupitia maonesho ya kibiashara na kwenye sherehe za kitaifa.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Mwanaidi Salehe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika uzinduzi huo, alisema masuala ya wanawake yapo chini yake hivyo atahakikisha anawasaidia kwa kila namna.

Katibu Mkuu huyo ambaye alichangia Sh milioni moja kusaidia umoja huo alisisitiza kuwa “lazima tuzipiganie haki zetu wanawake, tuelimishane na tupendane na tuanze kwa watoto wetu wa kike tuwape mafunzo bora na kuwalinda wasijiingize kwenye vitendo viovu kama kuepuka dawa za Kulevya”.

DSC_0302

Wageni waalikwa wakiipokea meza kuu.

DSC_0311

Meza kuu katika nafasi yao kutoka kushoto ni Mkurugenzi Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa FAWE, Bi. Khadija Ally Mohamed, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious, Bi. Umul-Kulthum Ansel (Madam Ummy), mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe pamoja na Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Uwezeshaji, Bi. Fatma Gharib Bilal.

DSC_0318

Mshehereshaji kwenye uzinduzi wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious, Bi. Fauziat Abood.

DSC_0360

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious, Bi. Umul-Kulthum Ansel (Madam Ummy), akisoma risala yake mbele ya mgeni rasmi na wageni waalikwa (hawapo pichani).

DSC_0379

Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe akitoa baraka zake kwenye uzinduzi wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious mjini Unguja.

DSC_0371

Makamu mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious Bi. Evelyne Wilson akiteta jambo na mjumbe wa Umoja huo Bi. Sheha Hilal.

DSC_0323

Pichani juu na chini Baadhi ya Wanawake wanaounda Umoja wa Zanzibalicious na wageni waalikwa wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mwenyekiti wa Umoja huo kwenye sherehe za uzinduzi wa kukata na shoka uliofanyika kwenye hoteli ya Ocean View Beach Resort mjini Unguja.

DSC_0327

DSC_0328

DSC_0393

Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe, akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious mjini Unguja.

DSC_0002

Cake maalum katika kusheherekea uzinduzi wa Zanzibalicious Women Group.

DSC_0405

Mgeni rasmi Bi. Mwanaidi Salehe akikata cake maalum iliyoandaliwa kusindikiza uzinduzi wa Umoja huo.

DSC_0410

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious, Bi. Umul-Kulthum Ansel (Madam Ummy), akimlisha kipande cha cake mgeni rasmi kama ishara ya kumshukuru kwa kushiriki nao katika uzinduzi wa Umoja huo.

DSC_0417

Mgeni rasmi Bi. Mwanaidi Salehe akimlisha cake mdau wa masuala ya wanawake Bi. Mariam Abdallah.

DSC_0419

Mshehereshaji Bi. Fauziat Abood akianzisha mnada kwa wageni waalikwa kwa kuuza kipande cha cake kwa shilingi 10,000/= kwa ajili ya kuchangia Umoja huo ambao Wanawake wa Umoja huo wamekuwa wakijichangisha fedha kutoka mfukoni mwao kwa ajili ya kuisadia jamii hususan wanawake na waathirika wa Madawa ya Kulevya.

DSC_0434

Kina baba nao walihamasika kuunga mkono zoezi hilo ambapo walilishwa vipande vya cake na mgeni rasmi Bi. Mwanaidi Salehe.

DSC_0439

DSC_0442

DSC_0452

Mmoja wa wadhaminiwa sherehe hizo kutoka kampuni ya FAITH Tours and Safaris akilishwa kipande cha cake na mgeni rasmi.

DSC_0456

Burudani kutoka COCONUT BAND ambayo ndio habari ya mujini visiwani Unguja chini ya usimamizi wa Mkurugenzi wake Bw. Raymond.

DSC_0485

Mshehereshaji Bi. Fauziat Abood akikteta jambo na mwimbaji taarab mkongwe Bi. Zuhura Shaabani.

DSC_0503

Mjumbe wa Umoja na Wanawake wa Zanzibalicious Sheha Hilal na Makamu mwenyekiti wa Umoja huo Evelyne Wilson wakimwaga manoti kwa mwimbaji mkongwe wa taarab mjini Unguja Bi. Zuhura Shaabani alipokuwa akitoa burudani kwa wageni waalikwa kwenye sherehe za uzinduzi wa Umoja huo.

DSC_0588

Uliwaidia ule wasaa wa mahanjumaati yaliyoandaliwa na hoteli ya Ocean View Beach Resort kwa wageni waalikwa.

DSC_0565

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Uwezeshaji Zanzibar, Bi. Fatma Gharib Bilal akiongoza meza kuu kupata Dinner kwenye sherehe za uzinduzi wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious.

DSC_0619

DSC_0618

Wageni waalikwa wakijisave msosi wa nguvu, chezea Unguja wewe kwa kukaangiza....!!!

DSC_0631

It's Dinner time... ndani ya hoteli ya Ocean View Beach Resort.

DSC_0641

Mshereshaji Bi. Fauziat Abood akiendesha harambee ya kutunisha mfuko wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicous kwa kunadi vitu mbalimbali kwa wageni waalikwa.

DSC_0660

Makamu Mwemyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Zanzibalicious Bi. Evelyne Wilson akizunguka kwenye meza za wageni waliohidhuria sherehe za uzinduzi wa umoja huo kunadi vitu mbalimbali.

DSC_0666

Mnada ukiendelea.

DSC_0672

Hili litamfaa mke wa wangu, zuri.....! Mambo ya LVD mjini Unguja....Baba akionekana kuvutiwa na pochi lililotengenezwa na kitenge wakati wa mnada.

DSC_0680

Madam Ummy nae akinadi T-shirt kwa mdau wa Fisherman Tours.

DSC_0691

Mr. Otembo aalinunua T-shirts hizo kwa Tshs 200,000/= katika kuchangia jitihada za Umoja huo kuwafikia jamii visiwani Unguja.

DSC_0464

Pichani juu na chini wageni waalikwa wakibadilishana mawazo na kufurahi wakati wa sherehe za uzinduzi wa Zanzibalicious Women Group.

DSC_0542

DSC_0535

Walipendezaje...!!

DSC_0540

DSC_0536

DSC_0529

DSC_0528

DSC_0723

Makamu mwenyekiti akitoa utambulisho wa Wanawake wanaounda Umoja wa Zanzibalicious kwa wageni waalikwa.

DSC_0790

Mgeni rasmi na meza kuu kwenye picha ya pamoja na Zanzibalicious Women Group.

ZANZIBALICIOUS KUWAKOMBOA WANAWAKE

Mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Bi. Mwanaidi Salehe akisaini kitabu cha wageni cha Umoja wa Wanawak... [Read More]