Google PlusRSS FeedEmail

NAPE NNAUYE ALIPOHUTUBIA GOMBANI YA KALE PEMBA (VIDEO)

[Read More]

  • Awataka wananchi kutokubali kuyumbishwa
  • Awaambia wananchi wa Pemba ,Muungano wa serikali mbili ni rahisi kuusimamia na kuzitatua changamoto zake kuliko wa serikali tatu.
  • Asema Viongozi wao wangekuwa wa kweli wangekuwa na makazi ya kudumu na wananchi wao katika kufanikisha maendeleo,badala  yake wamekuwa watu wa kuingia na kutoka hivyo kukosa muda wa kusimamia maendeleo ya wananchi.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye viwanja vya mkutano Gombani ya Kale akiongozana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Ndugu Vuai Ali Vuai tayari kwa kuhutubia wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai akihutubia wananchi wa Pemba kabla ya kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuhutubia wananchi wa mikoa miwili ya Pemba katika viwanja vya Gombani ya Kale.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Mikoa miwili ya Pemba na kuwataka kuwa makini na viongozi wenye kauli mbili mbili kwani hawana nia njema na maendeleo yao zaidi ya kujifikiria wao binafsi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wananchi kwenye viwanja vya mikutano vya Gombani ya Kale,Pemba na kuwaambia wananchi hao kuwa CCM itaenda sambamba na wapotoshaji wa ukweli.
 Wananchi wakionyesha ishara ya muundo wa Serikali mbili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya Gombani ya Kale,Pemba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Ndugu Shaka Hamdu Shaka na Viongozi wengine wa CCM Zanzibar wakionyesha ishara ya muundo wa Serikali mbili za Muungano wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika Gombani ya Kale.
 Mabinti wa UVCCM Pemba wakisoma utenzi wa kumkaribisha KatibuMkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  kutoka kushoto ni Fatuma Juma Ramadhani na Halima Juma Haji kwenye viwanja vya Gombani ya Kale.
 Sheikh Hamisi Ali Hamisi akisoma dua kabla ya kuanza kwa mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Gombani ya Kale Pemba ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alihutubia umati.
 Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Ndugu Shaka Hamdu Shaka akihutubia wakazi wa Pemba na kuwaambia wawe makini na viongozi wanafiki wa kisiasa.
Makamu Mwenyekiti wa UWT Bi. Asha Bakari Makame akihutubia wananchi wa mikoa miwili ya   Pemba na kuwaambia kuwa wananchi wawe makini na viongozi wanaotaka kuvuruga Muungano wetu.

KINANA ATOA SOMO PEMBA

Awataka wananchi kutokubali kuyumbishwa Awaambia wananchi wa Pemba ,Muungano wa serikali mbili ni rahisi kuusimamia na kuzitatua changamoto ... [Read More]


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege Pemba, Katibu Mkuu anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara Pemba
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  akisalimiana na Viongozi wa CCM Pemba mara baada ya kuwasili Pemba leo ambapo anatarajiwa kufanya mkutano wa hadhara utakaofanyika Gombani ya Kale.
 Msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukikatiza mitaa ya Madungu Flat.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini vitabu vya wageni kwenye afisi kuu ya CCM Pemba Chake Chake pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wengine ofisini ni Naibu Katibu Mkuu CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai,Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kusini Ndugu Abdala Mshindo na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Ndugu Mzee Mbelwa.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiangalia Buku la Wageni ( Kitabu cha Kusaini Wageni) cha Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Pemba
Buku la Wageni ( Kitabu cha Kusaini Wageni) cha Afisi Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Pemba

KINANA AWASILI PEMBA

  Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (ZNZ) Vuai Ali Vuai mara baada ya kuwasili kwenye uwan... [Read More]

Na Mwandishi Maalum, New York
Tanzania  imeendelea kusisitiza kwamba,   nchi ambazo hazina mpango wa kuwa na silaha za nyukilia basi ziwe na haki ya kutumia  nyukilia kwa matumizi salama, na pia kupewa misaada ya kiufudi na uwezeshwaji katika eneo hilo.

Hayo yameelezwa na  Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Ramadhan Mwinyi wakati alipokuwa akitoa  maoni ya  Tanzania katika  mkutano wa  Kamati ya Maandalizi kwaajili ya mkutano  utakaofanyia tathmini   utekelezaji wa Mkataba wa kuzuia usambazaji holela wa silaha za  nyukilia ( NPT).

 Tanzania inashiriki kikamilifu katika Mkutano huo wa maandalizi ambao ni wa wiki mbili  na  unafanyika  Hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.  Wanaoshiriki  mkutano huu ni  nchi wanachama wa NPT pamoja na wawakilishi wa  mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs).

Dhumuni la mkutano huu wa maandalizi, ni kuaanda dondoo na mapendekezo    yatakayojadiliwa  katika mkutano wa tathmini kuhusu NPT. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika  mwakani (2015).
Akizungumza kwa  niaba ya  Tanzania,  Naibu Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Ramadhan Mwinyi, amesema, kama  Tanzania na kama ilivyo kwa mataifa mengi ingepeda kuona  silaha za nyukilia zinatoweka katika  uso wa dunia. Lakini inaamini kwamba kila nchi Tanzania ikiwamo  inayo haki ya  kuwa na fursa ya kutumia nyukilia kwa masuala  salama.

Mwakilishi huyo wa Tanzania, amebainisha kwamba, hakuna asiyetambua  madhara ya silaha  za nyukilia kutokana matukioa kadhaa mbayo  yametokea huko nyuma yakiwamo ya   Hiroshima.
Akatahadharia kwamba kuna dalili  za wazi ya kujirudia kwa madhara hayo kwa kile alichosema  Jumuiya ya kimataifa  na hasa kwa nchi ambazo zimejilimbikizia silaha hizo hazitaki konyesha nia ya kweli ya kuachana nazo.

Akasema,  inasikitisha kwamba yale mataifa ambayo yana malimbikizo ya silaha hizo, yameendelea kushikilia misimamo yao na hata kufikia mahali  pa  kutetea uhalali wa kuwa na silaha hizo.

Tanzania ikaeleza kwamba,  silaha za nyukilia si tisho kubwa kwa nchi za Afrika, kwani   tishio  kubwa na ambalo linachangia katika  uvunjifu wa Amani na upotevu wa  maisha ya watu ni silaha ndogo ndogo na  nyepesi na  siyo  silaha za nyukilia.

Balozi Mwinyi amewahoji washiriki wa mkutano huo,   kwamba   ni  dunia ya aina gani  tunayotaka  kuwarithisha watoto wetu kwa kuendelea  kukumbatia silaha hizo za maangamizi.

 Akabainisha kwamba Tanzania  inaamini katika  Mkataba huo wa NPT kwa kile alichosema utekelezaji wake utaifanya dunia kuwa mahali salama. Na kwamba licha ya  kuridhia  mkataba huo, Tanzania pia   ni mwanachama wa mikataba mingine ya  kikanda  inayohusu uthibiti wa silaha za nyukilia. Hotuba Kamili ya Balozi Mwinyi>BOFYA HAPA

TANZANIA YATAKA MATUMIZI SALAMA YA NYUKILIA YASIZUIWE

Na Mwandishi Maalum, New York Tanzania  imeendelea kusisitiza kwamba,   nchi ambazo hazina mpango wa kuwa na silaha za nyukilia basi ziwe ... [Read More]

MALKIA wa muziki wa Injili nchini Afrika Kusini, Rebecca Malope anatarajiwa kutua kwenye jiji la Mwanza a.k.a ROCKY CITY  April 4,ikiwa ni sehemu ya muendelezo wa Tamasha la Pasaka 2014

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama amesema kuwa Nyota huyo wa muziki wa nyimbo za Kiroho,ni miongoni mwa wasanii watakaotumbuiza kwenye Tamasha hilo,ameeleza kuwa msanii huyo alipata kura nyingi kutoka kwa mashabiki waliompendekeza kutumbuiza jijini humo.

“Tunashukuru kwamba baada ya mapendekezo ya mashabiki tuliwasiliana na Rebecca ambaye ameonesha uungwana wa hali ya juu na kutukubalia ombi letu. 

“Lakini pamoja na kukubali ana ratiba ya maonesho sehemu nyingine huko kwao, hivyo ametuambia hatatumbuiza katika mikoa yote ambayo tamasha litafanyika mwaka huu, hivyo tutaangalia wapi tumpangie kulingana na ratiba yake. 
 
“Lakini niwahakikishie mashabiki wetu kwamba msanii huyo tutakuwa naye na sasa ni suala la Kamati ya Maandalizi kuona ratiba yake ilivyo na kisha nasi tumuweke kwenye ratiba yetu ili mashabiki wafurahi,” alisema Msama. 

Rebecca amewahi kutamba na albamu za Saturday Nite (aliyoitoa Januari 1, 2009), Hlala Nami (Novemba 11, 2003), Siyabonga (Desemba 21, 2000), Free at Last (Novemba 18, 1997), African Classics (Mei 5, 2009) na Greatest Hits (Januari 10, 2006).
Wasanii wengine watakaotumbuiza kwenye tamasha hilo ambao tayari wameshathibitisha ni Upendo Nkone, John Lissu, Upendo Kilahiro, Rose Muhando na waimbaji wengine ambao inaelezwa watatajwa hapo baadae.

MWENDELEZO WA PASAKA;MWANAMUZIKI REBECCA MALOPE KUTUMBUIZA APRIL 4 JIJINI MWANZA

MALKIA wa muziki wa Injili nchini Afrika Kusini, Rebecca Malope anatarajiwa kutua kwenye jiji la Mwanza a.k.a ROCKY CITY  April 4,ikiwa ni... [Read More]

GESI KUPEWA KIPAUMBELE BAJETI YA 2014/15

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusianona Uratibu, Stephen Wasira, akisoma rasimu ya Bajeti ya mwaka 2014/20015, jijini Dar es Salaam Waziri... [Read More]


 Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.Evarist Welle Ndikilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza ,matembezi hayo yalihitimishwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
 Wafanyakazi wa Mkemia Mkuu wa Serikali wakiingia uwanjani CCM Kirumba Mwanza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza .
 Wafanyakazi wa Idara ya Maliasili wakiingia uwanjani CCM Kirumba katika kuhitimisha siku ya wafanyakazi..
 Mahakama ya Tanzania wakiingia uwanja wa CCM Kirumba huku wakitanguliza ujumbe mzito.
 Kibanda cha Veta kilikuwa moja ya vibanda vilivyovutia kwenye maonyesho ya Siku ya Wafanyakazi zilizofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza.

 Wafanyakazi wa Hospitali ya Bugando wakielekea kuingia kwenye matembezi ya mshikamano katika kusheherekea siku ya Wafanyakazi kwenye Viwanja vya CCM Kirumba.
Wafanyakazi wa Halmashauri ya Jiji Mwanza wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.Evarist Welle Ndikilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi mkoa wa Mwanza ,matembezi hayo yalihitimishwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba.

SHEREHE ZA MEI MOSI MWANZA ZAFANA

  Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakipita ya mgeni wa heshima Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Eng.Evarist Welle Ndikilo wakati wa maadhimi... [Read More]