Google PlusRSS FeedEmail

KINANA : WATENDAJI FIKISHENI TAARIFA KWA WAKATI

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimuinua mtoto juu ambaye alikuja kwenye mapokezi wakati wakiwasili wilaya ya Meatu.
 Katibu Mkuu wa CCM Taifa  ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki zoezi la kupiga lipu jengo la ofisi ya chama kata ya Ng'oboka wilayani Meatu ikiwa moja ya majukumu yake ya kukagua uhai wa Chama.
 Katibu Mkuu akishiriki kupasua ubao baada ya kushiriki kufungua shughuli za wajasiriamali wa Vijana Kata ya Bomani.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Balozi wa Shina namba 31 Itinje Silasi Mhandi ikiwa sehemu ya ziara yake ambapo amekusudia uwatembelea mabalozi mbalimbali.
 Katibu Mkuu ndugu Abdulrahman Kinana akikagua daraja la mto Mwahnuzi ambalo ni sehemu ya ahadi za Rais Jakaya Kikwete.
 Daraja la mto Mwahnuzi likiwa limekamilika kabisa.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kujenga uzio wa kuzuia mmomonyoko kandokando ya daraja la mto Mwahnuzi.
 Nyumba mpya za watumishi wa halmashauri ya wilaya ya Meatu.
  Katibu Mkuu wa CCM akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiangalia nyumba zinazojengwa kwa ajili ya watumishi wa Halmshauri,wilayani Meatu.
 Wakazi wa wilaya ya Meatu wakigombea bendera za CCM kutoka kwa Mkuu wa wilaya ya Meatu Rosemary Kirigini.

 Sehemu ya Umati wa watu uliofurika kwenye viwanja vya kitua cha mabasi cha Mwahnuzi wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 
 Katibu Mkuu wa CCM ndugu Abdulrahman Kinana akiwa na mavazi yake ya kichifu baada ya kusimikwa rasmi na sasa anatambulika kama Chifu Kilabanya.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akihutubia wakazi wa Meatu katika viwanja vya Mwahnuzi wilayani hapo ambapo aliwasihi sana wananchi kuwa makini na vibaraka wa siasa wanaotaka kuvuruga mchakato wa Katiba.
 Ktibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimsaidia mlemavu Daud Deus ambaye alikabidhiwa baiskeli ya miguu mitatu na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Mbunge wa Maswa John Shibuda akizungumza na mwananchi wakati wa mkutano wa hadhara wa CCM ambapo aliwaambia wananchi yeye na Kinana ni marafiki wakubwa na wamesoma pamoja na pia Nape ni mtoto wake kwani yeye na baba yake Nape walikuwa maswahiba sana.

This entry was posted in

Leave a Reply