Google PlusRSS FeedEmail

VYAMA VYASHAURIWA KUWATUMIWA MAWAKALA WA JIMBO HUSIKA



TUME ya Taifa ya uchaguzi imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kuhakikisha kuwa wanawatumia mawakala wanaotoka katika maeneo au vituo husika vya kupigia kura,ambao watawafahamua na kuwatambua wapiga kura wa eneo husika. 

Akizungumza katika mkutano baina ya vyama vya siasa na tume hiyo,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji mstaafu Damiani Lubuva amesema kuwa pamoja na kuwa sheria haikatazi kwa vyama kuteua mawakala wa vyama kutoka majimbo mengine ya uchaguzi,lakini ni vyema kuwateua wale wanaotoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura wao. 

“Kumekuwa na mazoea kwa baadhi ya vyama vya siasa kuteua mawakala wanaotoka majimbo mengine ya uchaguzi japokuwa sheria haikatazi lakini ni vema vyama vikatumia busara  ya kuwateua mawakala kutoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura”alisema Jaji Lubuva. 

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa wananchi kujitokeza kupiga kura,Lubuva alisema kuwa tume inatambua juhudi za viongozi wa vyama vya siasa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kushiriki katika uchaguzi lakini akawataka viongozi hao kuhakikisha kuwa wanawahamasisha zaidi wapiga kura kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura. 

Akizungumzia kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi huo mdogo wa Chalinze,Msimamizi msaidizi wa uchaguzi wa jimbo hilo,ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Samweli Sarianga alisema kuwa vifaa vyote na maandalizi yamekamilika japokuwa kumekuwako na changamoto nyingi ikiwamo uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni na kusisitiza kuwa iwapo hali ya hewa itakuwa ni nzuri basi kuna uhakika wa vifaa vyote vya uchaguzi vitakuwa vimefikishwa katika maeneo husika tayari kwa ajili ya kusambazwa katika vituo vya kupigia kura. 

Jumla ya vyama 5 vinatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo mdogo wa Chalinze ambapo lina idadi ya wapiga 92,939,ambapo vyama hivyo ni CCM,CHADEMA,NRA,CUF na AFP

This entry was posted in

One Response so far.

  1. Na ndio maana yame haiwezekani wakala atoke nje ya jimbo husika.
    Umeelewa jaji.((

Leave a Reply