Google PlusRSS FeedEmail

HABARI ZA MAGAZETINI LEO JUMANNE TAREHE 23TH APRIL 2013.


IMETAYARISHWA NA MWENDA SULIMAN

UHURU:
SERIKALI KUSAMBAZA SEMBE
Kinu cha iringa kutumika
CAG akabidhiwa rungu
VIONGOZI AFRIKA MSITUMIWE
Rais Jakaya Kikwete amewataka viongozi wa Afrika kutokubali kutumiwa na kusababisha migogoro hususan inayotokana na mipaka au ukabila.
POLISI: UPELELEZI KESI YA LWAKATARE UMEKAMILIKA.
(Habari hii imesharipotiwa)
KORTI YABAINI KASORO KESI YA AKINA ZOMBE
(Habari hii imesharipotiwa)
DR SHEIN ATAKA MAFANIKIO ZAIDI CCM
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Rais Alli M Shein amewataka wanaCCM kuhakikisha chama kinapata mafanikio na kushinda kila ifikapo  kipindi cha uchaguzi mkuu.
MAHAKAMA YATUPA HOJA ZA MAKADA
(habari hii imesharipotiwa)
WAZIRI HAWA AKEMEA MAMEYA, WENYEVITI.
Waziri wan chi, ofisi ya waziri mkuu TAMISEMI Hawa Ghasia amewaonya mameya na wenyeviti wa halmashauri nchini kuacha kujihusisha na shughuli za kandarasi za miradi.
MBUNE AMVAA OFISA USHIRIKA.
Mbunge James Lembeli amemlipua bungeni ofisa ushirika wa wilaya ya kahama, akidai ni kinara wa wizi wa fedha za wakulima wa tumbaku.
GHARAMA ELIMU YA JUU KUWEKEWA MIKAKATI
Serikali itawasilisha bungeni muswada wa sheria ya mfuko wa Elimu ya juu katika kikao kijacho.
Muswada huo unalenga kuweka utaratibu utakaowezesha kubaini vyanzo mbadala vya kugharamia elimu ya juu.
SERIKALI YAJIZATITI UKUSANYAJI MAPATO.
Serikali imesema inaendelea kutafuta njia za kuongeza vyanzo vyake vya mapato.naibu waziri wa fedha Janet Mbene alisema bungeni kuwa mafungu ya bajeti yataongezeka kwa kadri ya upatikanaji fedha.
UWEKEZAJI WA NJE WONGEZEKA
Mitaji ya uwekezaji kutoka nje ya nchi imeongezeka kutoka dola za marekani milioni 520 (shs bilioni nane) mwaka  2005 hadi dola bilioni 11 (shs trillion sita) mwaka 2011
JK AZINDUA UMOJA WA WAFANYABIASHARA
Rais Jakaya Kikwete amezindua umoja wa ushirikiano baina ya wafanyabiashara wa Tanzania na Uturuki.
Uzinduzi huo ulifanyika katika hafla iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita katika hotel ya Hyatt Kilimanjaro, jijini Dar es salaam.


HABARI LEO:
BEI YA CHAKULA SASA KUPUNGUA
Kampuni 300 zajitokeza kuzalisha kwa wingi
Kitauzwa nchini na ziada soko la kimataifa.
JALADA LA LWAKATARE KWA DPP
(Habari hii imesharipotiwa)
LEMA AIBWAGA TENA CCM KORTINI
Mahakama ya rufaa yakubaliana na kuu
Waliokata rufaa waamriwa kugharamia.
(habari hii imesharipotiwa\)
UKOLONI WACHANGIA MIGOGORO YA MIPAKA AFRIKA
Rais Jakaya kikwete ameshtumu serza za kikoloni akisema zimechangia migogoro ya mipaka katika baadhi ya ardhi za afrika.
BBADHI YA WABUNGE WA CCM WAKATAA KUIUNGA MIKONO BAJETI
(HABARI HII IMESHARIPOTIWA)
RAIS AMTEUA MKURUGENZI MTENDANI WA TIC
Rais Jakaya Kikwete amemteua Julieti kairuki kuwa kurugenzi mtendaki wa kituo cha uwekezaji.
RUSHWA YASHAMIRI SEKTA YA MANUNUZI:
Mamlaka ya udhibiti na usimamizi wa umma (PPRA) imesema vitendo vya rushwa katika sekta ya manunuzi ndani ya mamlaka mbalimbali zimeendelea kushamiri ka kiasi kukubwa.
USAFIRI WA UBUNGO WAREJEA.
Usafiri wa treni kati ya ubungo na stesheni umerejea tena jana huku abiria wachache wakijitokeza kupanda.
Usafiri huo ulisitishwa mwezi uliopita.
WANAFUNZI 3900 VYUO WAKOSA MIKOPO
(HABARI HII IMESHARIPOTIWA)
WIZARA YA KILIMO YAKAMILISHA ANDIKO LA VIJANA KUJIAJIRI.
Wizara ya kilimo, chakula na ushirika imekamilisha andiko la namna ya kuwavutia vijana kujiajirti katika kilimo na biashara.

TANZANIA DAIMA:
WATESAJI WA KIBANDA, ULIMBOKA KITENDAWILI
polisi wakosa majibu wadai uchunguzi unaendelea
lwakatere, Ludovick jalada lao lakabidhiwa kwa DPP.
Watesaji wa mwenyekiti wa jumuiya ya madaktari nchini, DR Ulimboka na mwenyekiti wa jukwaa la wahariri Kibanda bado kindawili baada ya polisi kudai inaendelea na uchunguzi
NJAA YATIKISA NUSU YA NCHI.
Halmashauri 70 kati ya 136 nchini, zinakabiliwa na janga la njaa kutokana na ukame uliosababisha uzalishaji kuwa mdogo.
LEMA AILIZA TENA CCM
(habari hii imesharipotiwa)
WANA-CUF 11 WAWANIA JIMBO LA CHAMBANI
Wanachama 11 wa CUF wamejitokeza kuwania ubunge katika jimbo la chambani lililo kisiwani Pemba, kutokana na kifo cha mbunge wake Salim Hemed Khamis.
DOSARI ZA HATI ZAKWAMISHA RUFAA YA ZOMBE.
Mahakama ya Rufaa nchini, jana ilishindwa kuanza kusikiliza rufaa iliyokatwa na mkurugenzi wa mashitaka (DPP) Dk Eliezer Feleshi.
WABUNGE WAMBANA WAZIRI WA KILIMO
(Habari hii imesharipotiwa)
USHIRIKINA WAZUA BALAA KWA PINDA
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya mizengo Pinda, kata ya kibaoni wilayani Mlele wamemshambilia kwa mawe na matofali mkuu wa shule hiyo na mwalimu wa taaluma  kisha kuharibu jengo la utawala na nyumba za walimu, wakiwatuhumu kujihusisha na vitendo vya uchawi.
WIZARA IPITIE SERA YA UENDESHAJI VYUO BINAFSI.
Wizara ya Elimu na mafunzo ya ufungi staid imetakiwa kupitia upya sera ya uendeshaji wa vyuo binafsi vinavyotoa mafunzo ya ualimu nchini ili kuviwezesha vyuo hivyo kutoa taaluma yenye tija.
WANANCHI WATAKIWA KUTOTISHWA NA WANAHARAKATI
Wananchi wanaoishi maeneo yaliyogunduliwa na kuwepo na madini ya uranium wametakiwa kutotishwa na maneno ya wanaharakati, kwani serikali haitayarutubisha madini hayo bali kuyachimba na kuyauza nje kama malighafi ili kuepuka madhara..
MAKALA_TENDWA ANALEA UCHOCHEZI WA CCM
Makala inataja matukio mbalimbali ya vyama vya upinzani kuhusishwa na udini na ukabila na kusababisha chuki miongoni mwa watu na kumtaka panda kuikemea CCM kuacha kueneza propaganda hizo chafu.
MNYIKA  ASUBIRI MKUTANO WA RAIS.
Ikulu imetakiwa kutoa ufafanuzi kuhusu mkutano uliokuwa ufanyike kati ya Rais Jakaya Kikwete na mbunge wa Ubungo John Mnyika.

MTANZANIA:
WABUNGE CCM WACHACHAMAA
Wajimbanga kukwamisha bajeti ya kilimo, Maige, lembele waongoza mashambulizi.
(habari hii imesharipotiwa)
POLISI: KESI YA LWAKATARE IMEIVA.
Jeshi la polisi nchini limetoa taarifa ya kukamilika kwa uchunguzi dhidi ya tuhuma za kuhusika na vitendo vya kigaidi zinazowakabili mkurugenzi wa ulinzi na usalama wa Chadema.
HOMA UCHAGUZI ,ADIWANI ARUSHA YAPANDA.
Mnyukano mkali wa kisiasa, unatarajiwa kuibuka tena juni mwaka huu kati ya CCM na CHADEMA,
TUME YA TAIFA YATANGAZA UCHAGUZI MDOGO CHAMBANI
(habari hii imesharipotiwa)
RUFANI DHIDI YA ZOMBE YAKWAMA.
(habari hii imesharipotiwa)
LEMA AWABWAGA TENA MAKADA WA CCM
(habari hii imesharipotiwa)
BENKI YA DUNIA YAOKOA BAJETI YA TANZANIA.
Tanzania imepokea mabilioni ya fedha kutoka benki ya dunia WB kwa ajili ya kusaidia bajeti ya 2013-2014 katika miradi ya umeme na gesi.
DC LUSHOTO AWAASA WAISLAMU
Mkuu wa wilaya ya lushoto, Alhaj Majid Mwanga amewataka viongozi wa dini ya kiislamu kuwaelimisha waumini wao kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo.
JUKWAA LA KATIBA LAWAPASHA WABUNGE.
M/kiti wa jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) Deus Kibamba amewapasha wabunge kwa kuwaambia kuwa wanapokuwa wakichangia mijadala bungeni wanajali zaidi maslahi ya vyama badala ya wananchi.
MNYIKA HAJARIDHIKA NA MAJIBU YA WASSIRA
Mbunge wa ubungo, John Mnyika (CHADEMA) amesema ofisi yake haijaridhika na majibu yaliyotolewa bungeni na waziri wan chi ofisi ya Rais (uhusiano na Uratibu) steven wassira kuhusu ahadya Rais Kikwete kukutana na mamlaka zinazosimamia huduma ya maji katika jiji la Dar es salaam.
SALMA KIKWETE AWAPA SOMO WANAUME
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amewataka wanaume kujenga tabia ya kuongozan ana wake zao wanapokwenda hospitalini kujiunga na uzazi wa mpango.
KINANA ATAFUTA SULUHU YA WAKULIMA, KIWANDA CHA MTIBWA
Katibu mkuu wa CCM ndugu A kinana amefanya mkutano wa pamoja kati ya wakulima na uongozi wa kiwanda cha mtibwa ili kutafuta suluhu ya mgogoro wao unaoendelea.



MWANANCHI:
LEMA KIDEDEA TENA
Dar es salaam; mbunge wa arusha mjini (chadema) Godbless Lema ameibuka kidedea baada ya mahakama ya rufani kutupilia mbali maombi ya marejeo ya rufaa iliyomrejesha bungeni. Maombi hayo yaliwaslishwa na makada watatu wa CCM mkoani Arusha ambao walitaka mahakama ifanye marejeo ya hukumu yake ya awali.
CHC WAKAIDI RIPOTI YA CAG
Dar es salaam: bodi ya shirika hodhi la mali za serikali (CHC)  imelikaidi bunge na kuendelea na utaratibu wa uuzaji wa kiwanja namba 10 kilichopo barabara ya nyerere, Dar es salaam.
BAJETI YA KILIMO: MAIGE, LEMBELI WAIBANA SERIKALI.
Dodoma: wakati Tanzania imetajwa kuwa nchi ya pili kwa umasikini kwenye ukanda wa Afrika Mashariki, wabunge wameishukia serikali kwa kutenga fedha kidogo kwenye bajeti ya kilimo.
KIKWETE: AFRIKA TUMEPIGA HATUA, TUNAWEZA KUJISIMAMIA.
Rais Jakaya Kikwete, amesema Bara la Afrika limepitia kwenye kipindi kigumu cha kukabiliana na utawala wa kikoloni ulioendesha mambo kwa kuzikandamiza nchi za kiafrika, lakini sasa bara hilo limepiga hatua na linaweza kuzitafutia ufumbuzi changamoto za kiusalama pasipo kutegemea msaada wa nje.
WABUNGE CHADEMA WAAHIDI KUSHAMBULIA KWA MIKUTANO
Dar es salaam: wabunge sita wa chadema waliosimamishwa siku tano kuhudhuria vikao vya bunge, leo wameanza kushambulia kwa mikutano yao katika jimbo la Iringa mjini baada ya kumaliza mwanza.
UPELELEZI KESI YA LWAKATARE UMEKAMILIKA-MKURUGENZI
Dar es salaam: Kaimu Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai nchini, Issaya Mulungu, amesema upelelezi kuhusu tuhuma za vitendo vya ugaidi zinazomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema Wilfred Lwakatare na mwenzake umekamilika.
RUFAA DHIDI YA ZOMBE NJIAPANDA
Dar es salaam: rufaa dhidi ya aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es salaam Abdalah Zombe na wenzake wanane, iko katika njiapanda baada ya Mahakama ya Rufani kuibua dosari za kisheria.
SERIKALI YAFUNGA VIWANDA VYA NONDO.
Ni baada ya kuthibitika kuwa nondo zinazozalishwa na viwanda hivyo hazina ubora unaokamilika.
UHURU WA HABARI KUADHIMISHWA.
Taasisi ya vyombo vya habari kusini mwa afrika tawi la Tanzannia litashirikiana na wadau mbalimbaliwa habari nchini kuandaa sherehe ya kuadhimisha miaka 20 ya siku ya uhuru
VICKY KAMATA AWAASA VIJANA KUHUBIRI AMANI
Geita|: mbunge wa viti maalum Geita,Vicky Kamata amewataka vijana kutumia nafasi zao kuliombea amani Taifa, kwani kuna baadhi ya watu wanataka kutumia umaarufu kuivuruga amani iliyopo.
MIKUTANO YA CHADEMA KUENDELEA IRINGA.
Iringa: CHADEMA leo kinatarajia kufanya mkutano wa hadhara uwanja wa mwembetogwa mjini hapa ukiwa ni mwendelezo wa mpango wao waliodai watawashitaki kiti cha spika kwa wananchi.  
BENKI YA DUNIA KUSAMBAZA UMEME BIHARAMULO VIJIJINI
Biharamulo: Benki ya dunia kwa kushirikiana na wakala wa umeme vijijini (REA) zinatarajiwa kusambazwa umeme kwa shule za sekondari sita.
3,800 WAKOSA MIKOPO KUSOMA ELIMU YA JUU
Jumla ya wanafunzi 3821 waliokuwa na sifa ya kwenda vyuo vikuu na kupata mikopo hawajapewa mikopo hiyo.
WAPINZANI WATAKA KUJUA MAFANIKIO YA KILIMO KWANZA
Kambi ya upinzanib imeitaka serikali kueleza kwa kina utekelezaji wa nguzo kumi za kilimo kwanza.

This entry was posted in

Leave a Reply