Google PlusRSS FeedEmail

CCM YAIFUNIKA MAKAMBAKO, WANANCHI WAFURIKA MKUTANO WA HADHARA WA KINANA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kimama akihutubia mamia ya wananchi waliofurika kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jioni hii kwenye Uwanja wa michezo mjini Makambako mkoani Njombe.
 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye akihutubia mkutano huo
 Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe, Deo Sanga akitoa yake ya moyoni mbele ya wananchi kabla ya kumkaribisha Kinana kuhutubia mkutano huo.
 Ilibidi badhi ya wananchi kuongeza urefu wao kwa kusimama kwenye baiskeli kuweza kuona kila kilichokuwa kikifanyika kwenye mkutano huo
 Msimamizi wa utekelezaji wa ilani ya CCM, wilaya ya Njombe, Mkuu wa wilaya hiyo Saraha Dumba, akikimbilia jukwaani alipotambulishwa uwepo wake kwenye mkutano huo.
Baadhi ya madiwani wilayani Njombe, wakinyoosha mikono walipotambulishwa uwepo wao kwenye mkuyano huo.
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi ya CCM, Edna Msigwa, alipokabidhi kadi kwa wanachama 150 wapya wa CCM katika mkutano huo. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Njombe, Deo Sanga aka Jah People.

 Wanachama wapya waliopewa kadi ya Kinana, wakila kiapo
 Wanachama hao wapya wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Adbulrahman Kinana na viongozi wengine alioambatana nao kwenye mkutano huo.
 Kabla ya kuwasili kwenye Uwanja wa mkutano huo, Kinana alikagua mabanda ya maonyesho ya wajasiriamali katika wilaya ya Njombe. Hapa alikuwa alitazama mafuta yanayosindikwa na wajasiriamali hao
 Mapema Kinana alizindua Ofisi ya CCM tawi la Mizani, wilayani Njombe.
Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akitabasam baada ya mkutano wake huo kufana vya kutosha. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

This entry was posted in

Leave a Reply