Google PlusRSS FeedEmail

NDEGE YA ETHIOPIAN AIRLINE YANUSURIKA AJALI YATUA GHAFLA UWANJA WA ARUSHA

Habari iliyotufikia kutoka Arusha leo ni kwamba Ndege ya Ethiopian Airline Boing 787 imetua ghafla katika Uwanja wa Ndege wa Arusha baada ya kushindwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa  Kilimanjari (KIA) ikitokea Ethiopia kwenda Afrika Kusini.

Ndege hiyo ilikuwa na abiria zaidi ya 200 na wafanyakazi tisa. kabla ya kupaa tena ilibidi abiria wote wateremke, na kupunguzwa mafuta ili kupunguza uzito wa ndege hiyo. Abiria waliamuriwa kwenda kupandia ndege hiyo kwenye Uwanja wa Ndege wa KIA.

This entry was posted in

Leave a Reply