Google PlusRSS FeedEmail

MAMBO YAMEIVA NDANI YA BANDA LA MeTL GROUP KWENYE MAONYESHO YA SABASABA!



DSC_0004
Muonekano wa lango kuu la kuingia ndani ya banda la Makampuni ya MeTL Group kwenye maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yaliyozinduliwa rasmi jana kwa kupewa baraka na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Sefu Iddi katika Uwanja wa Maonesho wa Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
DSC_0008
Utajiuliza kwani LG wapo ndani ya Banda la MeTL Group kwenye maonyesho ya Sabasaba kwa sababu MeTL Group wamekuwa Mawakala waliothibitishwa Tanzania nzima (Authorized Dealers) kuuza vifaa vya LG nchini. USISAHAU KUJINADIKISHA KWA AJILI YA DROO YA BAHATI NASIBU ITAKAYOCHEZESHWA TAREHE 7 MWEZI HUU NDANI YA BANDA LETU...!
DSC_0120
Kampuni ya MeTL Group inahusika pia na masuala ya Vitenge, Khanga, Mashuka na n.k Njoo upendeze mwanamke na vitenge bora na imara kutoka MeTL Group.....Sikukuu ya Eid ilee na maandalizi yawe mapema kabisa...!
DSC_0125
Wakazi wa jiji la Dar wakivinjari ndani ya Banda la Mohammed Enterprises Tanzania Ltd. (MeTL Group) kujipatia mahitaji mbalimbali za bidhaa bora kabisa kwa bei nafuu msimu huu wa Sabasaba.
DSC_0151
Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar wakiangalia na kupata maelezo ya bidhaa mbalimbali kama TV, Music System, Simu za mkononi za nyingine nyingi kutoka kampuni ya LG ambapo MeTL Group ndio Authorized Dealers pekee nchini Tanzania.
DSC_0124
Muonekano wa ndani wa Banda letu la MeTL Group ukiwa umenakshiwa kwa mabango pamoja na TV za LG zinazoonyesha matangazo mbalimbali ya bidhaa zetu.
DSC_0136
Mmoja wa wateja akipata maelezo kutoka kwa wataalamu wetu waliobobea wa vipozi kwenye banda letu la MeTL Group.
DSC_0117
Watu wanatakaje kupendeza.....!! bado wewe tu hujajipatia kitenge chako na Khanga....kwa bei nafuu kabisa katika msimu wa Sabasaba.
DSC_0360
Baadhi ya ushers wanaotohuduma kwa wateja ndani ya banda la MeTL GROUP wakipozi kwenye Big Screen ya LG inayoonyesha tangazo la bidhaa mpya ya "MO BEAUTY SOAP" ambapo Balozi wake ni mrembo aliyewahi kushika taji la Miss Tanzania namba mbili JOKATE MWEGELO.

DSC_0238
Mmoja wa kikundi cha uhamasishaji kwenye banda la MeTL Group akikata kiu yake na kinywa chenye ladha tamu kabisa ambacho kitaingia sokoni hivi karibuni "MO Portello" kinachouzwa ndani ya banda hilo.
DSC_0240
Aaaah kinywaji safi kabisa...sasa nimekata kiu yangu...!! Unakaribishwa na wewe pia kukijaribu kinauzwa kwa bei nzuri kabisa ya offer katika msimu huu wa Sabasaba.
DSC_0242
Mimi napenda "MO Portello" wewe je....??
DSC_0292
AGRO MeTL wauzaji wa Mbolea na Matrekta ya kisasa ambayo ni imara na bora kwa mazingira yetu ya Tanzania yapo kwenye banda letu...Kilimo kwanza ndio mpango mzima...!!
DSC_0109
Mambo ya Katani yanahusika pia ndani ya banda la MeTL Group kwenye viwanja vya Sabasaba.
DSC_0131
Mambo ya Ugali, Maandazi na bidhaa mbalimbali za nafaka zinapatikana pia bila kusahau MO SEMBE..Unga safi kabisa wa kupikia.
DSC_0142
Mambo ya usafi pia yanahusika jamani eeeeh...Sabuni za kufulia za unga zenye kuondoa madoa sugu na uchafu wa aina zote zinapatikana pia wewe tu na pochi lako.
DSC_0224
Watoto wakipata maelezo kutoka kwa mhudumu wa vinywaji vya MeTL Group kwenye banda letu ndani ya maonyesho ya Sabasaba.
DSC_0236
Watoto wakipata Ukodak baada ya kuyakubali maji safi ya kunywa kwa gharama nafuu kabisa yanayotengenezwa na MeTL Group.
DSC_0253
Kata kiu yako kwa kujichagulia kinywaji ukipendacho hapa ndani ya banda la MeTL GROUP.
DSC_0345
Mmoja wa wateja akiangalia tangazo la bidhaa mpya ya MO BEAUTY SOAP ambapo Balozi wa sabuni hiyo ni mrembo aliyewahi kushitaji la Miss Tanzania namba mbili JOKATE MWEGELO.
DSC_0332
DSC_0113
Mfanyakazi wa MeTL Group akitoa maelezo ya ubora wa maji safi ya kunywa yenye viwango vya kimataifa. Unakaribishwa sana kuuliza maswali mbalimbali ndani ya banda letu.
DSC_0264
Kikundi cha NOMA SANA Group kikitoa burudani nje ya banda la MeTL Group kuwatumbuiza wakazi wa jiji wanaotembelea maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Sabasaba yanayoendelea jijini.Kwa picha zaidi ingia hapa

This entry was posted in

Leave a Reply