Google PlusRSS FeedEmail

RAIS KIKWETE APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WANNE, AKUTANA NA WAZIRI WA ULINZI WA CHINA

Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Malaysia nchini Tanzania Mheshimiwa Ismail Salem. Baada ya kupokea rasmi hati hizo Rais Dkt. Kikwete alifanya mazungumzo na balozi huyo huko Ikulu tarehe 4.7.2014.
 Rais Kikwete akizungumza na balozi huyo baada ya kupokea hati
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Cote d’ Ivoire hapa nchini Mheshimiwa Georges Aboua na baadaye kufanya mazungumzo naye huko Ikulu Ikulu tarehe 4.7.2014.
Rais Dkr. Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Venezuela hapa Tanzania Mheshimiwa Thony Balza Arismend na baadaye Rais Kikwete alifanya mazungumzo na mgeni wake huko Ikulu tarehe 4.7.2014.
Rais Kikwete akizungumza na Balozi huyo mteule wa Venezuela
Rais Dkt. Jakaya Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule Mheshimiwa Ahmat Awad Sakine wa Chad hapa nchini tarehe 4.7.2014.
  Rais Kikwete akizungumza na Balozi huyo mteule wa Chad baada ya kupokea hati zake za utambulisho
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha kwa mazungumzo Waziri wa Ulinzi wa China Jenerali Chang Wanquan huko Ikulu tarehe 4.7.2014.
Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na  Waziri huyo wa Ulinzi wa China Jenerali Chang Wanquan huko Ikulu tarehe 4.7.2014. PICHA ZOTE NA JOHN LUKUWI

This entry was posted in

Leave a Reply