Google PlusRSS FeedEmail

KITUO CHA WAJARIAMALI WASOMI CHA CHENGDU CHAMKUNA KINANA

NA BASHIR NKOROMO, CHENGDU, CHINA
KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana amesema, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kitaihimiza serikali yake, kuiga mbinu zinazotumiwa na Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC) ya kuweka vituo vya vijana wajasiriamali wasomi, kuwezesha wanaomaliza elimu ya juu waweze kutumia vipaji vyao kujiajiri badala ya kusubiri kuajiriwa.

Tanzania ikifanikiwa kufanya hivyo, itajikomboa kwa kuwasaidia vijana wengi ambao baada ya kumaliza masomo huhangaika kutafuta kazi za kuajiriwa badala ya kijiajiri wenyewe kutokana na elimu, ujunzi na ubunifu walio nao.

Kinana alisema, hayo leo Machi 14, 2013 baada yeye na ujumbe wake wa watu 14, waliopo katika ziara ya siku kumi ya mafunzo nchini China, kutembelea Kituo cha vijana wajasiriamali cha Chengdu, jimbo la Sichuan na kushuhudia jinsi vijana wasomi walivyoweza kutumia vipaji vyao kujiajiri baada ya kukusanywa kwenye kituo hicho kinachoitwa, Chengdu Hich Tech Postgraduetes Enterpreneurial Park.

"Kwa kweli vijana hawa wanaonyesha umahiri mkubwa wa kutumia vipaji vyao, ni muhimu nasi tukaiga namna hii bora ya kuwaweka vijana pamoja, kwa sababu inasaidia kupunguza tatizo la ajira na pia kuleta faida kwa taifa", alisema Kinana.

Kinana alimwagiza Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Martine Shigela aliyeko kwenye msafara wake, kuwasiliana na uongozi wa kituo hicho ili kuona namna mbinu zinazotumika kuwakusanya vijana kwenye kituo hicho zitakavyoweza kufanyika Tanzania.

Katika ziara hiyo, Kinana na msafara wake, walivutiwa baada ya kushuhudia vijana wanavyobuni na kutengeneza vifaa vya  kielekroniki kama vya simu, redio, televisheni, na wengine kubuni katuni, michezo na manjonjo mbalimbali ambayo huwekwa katika kompyuta na simu za mkononi kwa ajili ya wenye vifaa hivyo kujiliwaza.

"Kwa hiyo zile 'game' ambazo huwa tunacheza kwenye simu zetu au kompyuta ndiyo hutengezwa hapa?," aliuliza Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Shigela.

Akizungumza wakati akitoa maelezo kuhusiana na kituo hicho, Mkuu wa Kituo hicho, Zheng Xiola alisema, vijana zaidi ya 100 wameweza kukusanywa kwenye kituo hicho kwa ajili ya kufanya kazi mbalimbali za ubunifu katika mambo ya teknolojia hasa kuhusu elekroniki.

Alisema, wakati wapo wanaobuni na kutengeza vifaa vya kielekroniki kama vya simu, redio, televisheni na vifaa vingine vinavyotumia umeme, wengine ni wabunifu na watengezaji wa vikatuni, michezo, na mamnjonjo mbalimbali kwa ajili ya kompyuta au simu.

Xiola alisema, kazi hizo zimewafanya vijana wengi wanaomaliza masomo ya elimu ya juu, kujiari kwa njia hiyo kwakuwa kazi zao huuzwa ambapo kwa wale wanaotengeneza katuni, michezo na manjonjo ya kwenye simu au kompyuta huweza kuuza kwa kampuni zinazoteneza vifaa hivyo na wanaotengeneza vifaa vya kielekroniki huweza kuuzia kampuni au watu binafsi.

Alisema, mpango huo umetengezwa na serikali ya Chama Cha Kimomunisti cha China, kwa kutengea fedha ambazo hukopeshwa wajasiriamali wanaotaka kujiunga.

Pamoja na kituo hicho, leo Machi 14, 2013, Kinana na ujumbe wake walitembelea pia maeneo mbalimbali katika mji wa Chengdu kwa lengo la kuona na kujifunza fursa zipi CCM inaweza kuielekeza serikali yake, kuzifanya kwa ajili ya kuwezesha Tanzania kuinuka kiuchumi kama nchi na pia wananchi wake kwa jumla.

Baada ya kituo hicho, walitembelea eneo la kumbukumbu la Kihistoria la Jin Sha kuona namna ambavyo kumbukumbu zinatunzwa kwa njia bora zaidi ili kuwa na manufaa kwa taifa na dunia kwa jumla, pia walitembelea eneo la kiutalii la kihistoria ya zaidi ya miaka 100 iliyopita la  Kuan and Zai Culture alley ambako kuna majengo na mandhari ya amiaka mingi ambayo huvuta walii.

Baadaye Kinana alikutana na Naibu Katibu Mkuu wa CPC jimbo la Sichuani Zang Ning, na kuwa na mazungumzo naye kabla ya chakula cha jioni katika hoteli ya Jinjiang mjini Chengdu.

This entry was posted in

Leave a Reply