Google PlusRSS FeedEmail

ZIARA YA KIKAZI YA VIONGOZI WA UVCCM MKOANI MOROGORO

  KATIBU Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) Martine Shigela akifungua shila la wakereketwa wa umoja wa huo la waendesha Bodaboda wa Melela Kololo. Mvomelo mkoani Morogoro, leo Machi 2, 2013. Wapili kushoto ni Katibu wa UVCCM mkoa wa Morogoro, Jumaane Kitundu na Kulia ni Mjumbe wa Baraza la Vijana Morogoro Abubakar Assenga na Juliana Shonza aliyekuwa Makamu Mwenyekiti Taifa wa Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) ambaye amehamia CCM hivi karibuni.
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Martine Shigela akimkabidhi kadi ya UVCCM, dereva wa Bioda boda Stanslaus Mdumbwa, katika mkutano wa hadhara wa UVCCM uliofanyika Kijiji cha Melela, Wilayani Mvomelo mkoa wa Morogoro leo, Machi 2, 2013. Juma ya wanachama wapya 65 wa UVCCM walipewa kadi na Shigela. Wapili kushoto ni Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Jumanne Kitundu.
 4. Aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (BAVICHA) Juliana Shonza ambaye amekihama chama hicho hivi karibuni, akizungumza kwenye mkutano wa hadhara wa UVCCM, uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashada, Kilombero mkoani Morogoro, jana, Machi Mosi, 2013.
 "CCM IMEFANYA MENGI", Mzee wa Juma Jumaa mwenye umri wa miaka 80, akitoa ushuhuda huo, kwenye Mkutano wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) uliofanyika kwenye Uwanja wa Mashada, Kilombero mkoani Morogoro, jana, Machi Mosi, 2013. Kushoto ni Katibu wa Uchumi na Fedha wa UVCCM Makao Makuu, Omari Suleiman na Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa CCM mkoa wa Morogoro,  Abubakar Assenga.
 6. VIJANA wa hamasa wa UVCCM, wilaya ya Kilombero mkoa wa Morogoro, wakihanikiza shamrashamra wakati wa mkutano wa UVCCM uliofanyika Uwanja wa Mashada wilayani humo.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigela akimsaidia kupigangoma, Nyandelo Omari wakati wa mapokezi yake, katika kata ya Melela Mvomelo mkoani Morogoro alipowasili kwa ajili ya mkutano wa hadhara leo, Machi 2, 2013.
 Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro Sixtus Mapunda (kushoto) akitaniana jambo na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini, Juma Borafya nje ya Morogoro Hotel, jana kabla ya viongozi mbali mbali wa Umoja wa Vijana na wadau akiwemo Borafya kutawanyika katika maeneo mbalimbali mkoani Morogoro kwa ajili ya mikutano ya hadhara ya kuimarisha  Jumuia hiyo na CCM. Ziara.
 Kutoka kulia ni Mtera Mwampamba na Juliana Shonza waliohama kutoka Chadema hivi karibuni, wakiwa na viongozi wa UVCCM  Abubakari Assenga na Tumaini wa makao Makuu ya UVCCM Dar es salaam, kabla ya kuanza ziara hiyo mkoani Morogoro.
 Mjumbe wa NEC, Jonas Nkya akizungumza kwenye mkutano wa UVCCM uliofanyika jana Kilombero
 Shamra shamra zikihanikizwa wakati wa uzinduzi wa tawi la UVCCM,  Nyandelo Kilombero
 Mbunge Abdul Mtegete wa Kilombelo akizungumza kwenye mkutano wa UVCCM uliofanyika katika mji huo mdogo wa Kilombero jana. Karibu yake ni Assenga wa UVCCM
CCM MAMBO SAFI: Mwampamba aliyehama Chadema hivi karibuni akiwa amepozi picha na Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Morogoro,  Harrieth Suta nje ya hoteli ya Morogoro jana

This entry was posted in

Leave a Reply