Google PlusRSS FeedEmail

VIONGOZI WA CHAMA NA SERIKALI WAHUTUBIA WANANCHI WA KATAVI LEO

Katibu wa Halmashauri Kuu Taifa-Itikadi na Uenezi, Mh. Nape Nnauye akisalimiana na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi wa wilaya ya Mpanda, mkoa wa Katavi.
Viongozi wakuu wa Chama cha Mapinduzi wakishiriki maandamano kuelekea kwenye uwanja wa Kashaulili wilaya ya Mpanda.

Wapenzi na wanachama wa CCM wa Mkoa wa Katavi wakiwaongoza viongozi wa chama na serikali kwenye uwanja wa Kashaulili wilaya ya Mpanda ambapo viongozi hawa watahutubia na kuambia wananchi utekelezaji wa ilani ya CCM.
Mh.Nape akihutubia wananchi wa Mpanda waliofurika kwenye  uwanja wa Kashaulili,ambapo alikemea vikali vitendo vya vyama vingine kuendekeza vurugu badala ya siasa.
Mh.Mwigulu Mchemba akieleza wananchi masuala muhimu ya kiuchumi na kwa nini kunakuwa na mfumuko wa bei,pia alitumia fursa hiyo kukemea mauaji yalotokea kwenye jimbo lake ambapo kijana mmoja kiongozi wa chama aliuawa na wanachama wa chama cha upinzani.
Waziri wa Maji Prof.Jumanne Maghembe akihutubia wananchi wa Mkoa wa Katavi, ambapo ameahidi kulitatua tatizo la maji haraka iwezekanavyo na pia kutoa tamko la kushushwa kwa bei za maji.

Naibu Waziri Wizara ya Uchukuzi,Mh. Charles Tizeba akizungumzia masuala ya kuimarisha reli na pia  utunzaji wa treni zetu ikiwa suala zima la usafi, pia aliwaambia wananchi serikali imeagiza mabehewa ya abiria na ya mizigo.
Naibu Waziri Kilimo na chakula,Mh. Adam  Malima akihutubia wananchi wa mkoa wa Katavi, juu ya masuala mabali mbali ambayo yametekelezeka likiwemo suala la umeme na pia aliwaambia wakulima kwamba serikali imeandaa utaratibu mzuri wa vocha za kilimo ambazo utatangazwa hivi karibuni.
Naibu Waziri TAMISEMI,Mh.Aggrey Mwanri akihutubia wananchi wa Mpanda mkoani Katavi,ambapo aliwasihi kutokubali kudanganywa danganywa na pia aliwaambia wananchi serikali hii isingependa kuona wananchi wa chini akionewa, hivyo alitoa tamko la kutowalipisha ushuru wakina mama wafanya biashara ndogo ndogo mfano vitumbua na chapati.

This entry was posted in

Leave a Reply