Google PlusRSS FeedEmail

SHEREHE KUBWA ZA KUPONGEZA UONGOZI MPYA WA CCM KURINDIMA ZANZIBAR LEO

Makamu Mwenyekitin wa CCM, Dk. Shein
NA BASHIR NKOROMO, ZANZIBAR
Maelfu ya Wana-CCM na wananchi kwa jumla, wanatarajiwa kufurika leo kwenye Viwanja vya Demokrasia (zamani, Kibandamaiti), wakati wa sherehe kubwa ya kupongeza safu mpya ya uongiozi wa CCM kitaifa uliochaguliwa wakati wa mkutano mkuu wa CCM ulimalizika juzi juzi mjini Dodoma.

Kulingana naratiba iliyopatikana, sherehe hizo zitarindima kuanzia saa tisa alasiri, na safu karibu yote ya uongozi huo itakuwepo, isipokuwa mwenyekiti wa CCM, Taifa, Rais Jakaya Kikwete na Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Philip Mangula.

Imethibitishwa kwamba, kwenye sherehe hizo watakuwepo Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara) Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, Naibu Katibu Mkuu (Bara) Mwigulu Nchemba, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Vuai Ali Vuai, Katibu Mwenezi wa CCM, Nape Nnauye, Katibu wa Uchumi na Fedha Zakia Meghji, Katibu wa NEC Oganaizesheni Mohammed Seif Khatib na Katibu wa NEC, Siasa na mambo ya Nje, Dk. Asha-Rose Migiro.

This entry was posted in

Leave a Reply