Google PlusRSS FeedEmail

MAOFISA HABARI NA MAWASILIANO WATOA MSAADA KWA WAZEE WA KITUO CHA MWANZANGE, TANGA

Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Assah Mwambene, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania Innocent Mungy (mwenyeshati la mistari) na Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni toka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko (katikati) wakimkabidhi  kiroba cha mchele  moja ya Wazee wa Kituo cha Mwanzange Mkoani Tanga, ikiwa ni sehemu ya msaada uliotolewa na Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali katika kikao kazi kinachoendelea Mkoani humo.
Mkurugenzi wa Idara ya Utamaduni toka Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko akimkabidhi Afisa Ustawi wa Jamii anayesimamia kituo hicho cha wazee Bi Otilia Daniel fedha za kununulia mahitaji mengine wakati wa ziara ya kutoa msaada katika kituo hicho leo Mkoani Tanga.
 Nyumba za Makao ya Wazee za Mwanzange Mkoani Tanga.
Baadhi ya Maafisa Habari na Mawasiliano waliotembelea kituo cha wazee cha Mwenzange Mkoani Tanga
Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wazee wa kito cha Mwanzange ambapo walitoa Unga sembe Kilo 200, mchele kilo 300, mafuta ya kupikia dumu 2, mafuta ya kupaka, dawa za meno, chumvi, sukari, maharage,  nyama, majani ya chai, kanzu, misuli pamoja na nguo za kinamama.
(Picha Na Hassan Silayo)

This entry was posted in

Leave a Reply