Google PlusRSS FeedEmail

TBL YAKABIDHI WODI YA WAZAZI NA MIUNDOMBINU YA MAJI ILIYOKARABATIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA YA AMANA, ILALA


 Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) Kanda ya Ilala, Jesca Njau (kushoto) akikata utepe ikiwa ni ishara ya kukabidhi wodi ya watoto wachanga Katika Hospitali ya Rufaa ya Amana Ilala iliyokarabatiwa kwa msaada kampuni hiyo, Dar es Salaam jana.  Wanaoshuhudia kutoka kulia ni Daktari Bingwa wa Watoto wa Hospitali hiyo, Dk. Mtagi Kibatala, Mhandisi wa TBL, John Malisa na Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Meshack Shimwela. TBL ilitumia sh. mil. 68 kukarabati wodi hiyo na miundombinu yake. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Jesca Njau akipongezwa na Daktari Bingwa wa Watoto wa Hospitali hiyo, Dk. Mtagi Kibatala,
 Dk. Kibatala akitoa shukrani kwa TBL kwa msaada huo ambao alidai umepunguza kwa asilimia kubwa kupunguza adha kwa wazazi waliozaa watoto njiti.

 Mganga Mkuu wa Hospitali hiyo, Dk. Shimwela akitoa shukrani kwa TBL kwa msaada huo mkubwa wa ukarabati wa wodi ya wazazi na miundombinu ya maji.
 Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu  akielezea mikakati ya kampuni hiyo katika kusaidia jamii katika sekta ya maji, ambapo katika mkoa wa Dar es Salaam TBL imetumia sh. mil 450 kuboresha sekta ya maji katika vituo mbalimbali vya afya.
 Mzazi alyejifungua mtoto njiti Mariam Mbwambo, akitoa shukurani kwa TBL kwa msaada huo ambao alisema umesaidia kupunguza kero waliyokuwa wanaipata kukaa na watoto hao ambao wanahitaji uangalizi mkubwa.
 Mkazi wa Msimbazi Bondeni, Febi Joramu akitoa shukrani kwa TBL kwa msaada huo muhimu wa wazazi.
 Jesca Njau akizungumza na Mariamu baada ya kukabidhi eneo hilo lililokarabatiwa.
                                                   Moja ya vyoo vilivyokarabatiwa
 Sehemu ya mabomba yiliyokarabatiwa

Muuguzi Kiongozi wa Wodi ya Wazazi, Mercy Maleko akionesha choo kilichokarabatiwa cha watumishi wa wodi hiyo.

This entry was posted in

Leave a Reply