Google PlusRSS FeedEmail

TANGAZO LA MKUTANO WA HADHARA WA CHAMA CHA MAPINDUZI UTAKAOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA JANGWANI, SIKU YA JUMAMOSI, TAREHE 09-06-2012.


TANGAZO:

Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kimeandaa Mkutano Mkubwa wa Hadhara kwa wananchi wote, Siku ya Jumamosi, tarehe 09/06/2012, Katika Viwanja vya Jangwani Kuanzia saa 8 mchana. 
  Maudhui;  “ Kutoa Msimamo Wake Juu ya Masuala Yanayogusa Mustakabali wa Taifa. Hivyo Chama Kitatumia Fursa hiyo Kuelezea Watanzania Juu ya Msimamo Wake Katika Mambo yafuatayo:

1.     Hatma ya maisha ya Watanzania
·        Ajira
·        Miundo mbinu ya Barabara, Reli, Bandari Na Anga.
·        Bei za bidhaa mbalimbali.
·        Umeme
·        Rasilimali za taifa

2.     Msimamo wa Chama Cha Mapinduzi kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya.

3.     Vurugu za Zanzibar.


Katika Mkutano huo, Viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali watakuwepo na kutoa ufafanuzi juu ya masuala hayo yaliyoainishwa kama msimamo wa Chama Cha Mapinduzi.

Chama Cha Mapinduzi, kinawaalika wanachama wake wote, wakereketwa na wananchi kwa ujumla kuhudhuria katika mkutano huo mkubwa. Mkutano utafanyika kwa amani na utulivu na wote mnakaribishwa.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI
Imetolewa na:

JUMA SIMBA
KATIBU WA SIASA NA UENEZI
MKOA WA DAR ES SALAAM.
07/06/2012

This entry was posted in

Leave a Reply