Google PlusRSS FeedEmail

BUNGE LA BAJETI LAANZA LEO

Spika wa Bunge Anna Makinda
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo linaanza kikao chake cha Bajeti, ambapo muda wa kuchangia na kuwasilisha bajeti za wizara mbalimbali, umepunguzwa.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana, Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge, John Joel, alisema muda wa kuchangia Bajeti hiyo, umepunguzwa kutoka dakika 10 hadi saba na muda wa uwasilishaji wa bajeti za wizara mbalimbali, pia umepunguzwa.
Alisema kutokana na mabadiliko hayo, sasa kila wizara itapewa siku moja ya kuwasilisha bajeti yake na kujadiliwa. “Tumepima muda tukaona unatosha,“ alisema.

This entry was posted in

Leave a Reply