Google PlusRSS FeedEmail

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE URAMBO KWA KUHUTUBIA MKUTANO MKUBWA LEO KUFANYA ZIARA YA SIKU MOJA KALIUA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Urambo kwenye uwanja wa Wananchi na kuwaambia Serikali inatambua kero kubwa ya maji mkoani Tabora na mipango madhubuti ya kuwezesha kupunguza tatizo hilo inaendelea huku huduma ya mradi wa umeme vijijini itapatikana karibuni ikiambatana na Minara ya mawasiliano ya simu,lakini pia Katibu Mkuu aliwataka viongozi wa CCM kurekebisha kasoro zao na kutambua wajibu wao wa kuwatumikia wananchi ikiwa pamoja na kuisimamia serikali katika kutekeleza mipango ya maendeleo iliyoahidiwa kayika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Urambo na kuwaambia kuwa wawe makini na wasanii wa kisiasa ambao wamekosa sera na hoja zinazosaidia mwananchi wa kawaida katika kupambana na changamoto zinazomkabili.
 Mbunge wa Urambo Mashariki Ndugu Samuel Sitta akiwahutubia wakazi wa Urambo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa Wananchi,Urambo mkoani Tabora.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi pikipiki Katibu wa kata ya Ukondamoyo Baraka M.Baraka ,Piki piki 16 zimetolewa kwa kata zote 16 za wilaya ya Urambo na Mbunge wa Urambo Mashariki Samuel Sitta akishirikiana na Mbunge wa Viti maalum Magreth Sitta.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinanaakikabidhi baiskeli 95 kwa Makatibu wa Matawi CCM  ambazo zimetolewa na Mbunge Urambo Mashariki Samuel Sitta akishirikiana na Mbunge wa Viti Maalum Magreth Sitta.
 Vijana 90 wa CCM wilaya ya Urambo wakionyesha mshikamano wakati wakimpa salaam Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Adulrahman Kinana ikiwa pamoja na kumpongeza kwa kazi nzuri anayofanya katika kuimarisha chama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakishiriki kiapo wakati wa kuwaapisha wanachama wapya wa CCM wilaya ya Urambo ambapo watu 900 walijiunga na CCM.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na wazee wa kimila wa urambobaada ya kusimikwa rasmi kuwa Mzee wa kimila.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ,akiwa kwenye picha ya pamoja na wasanii wa kikundi cha Ugobogobo,wengine pichani ni Mbunge wa Urambo Mashariki Ndugu Samuel Sitta,Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwassa,Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Urambo Martha Faustine Susu,Mbunge wa Viti Maalum Magreth Sitta na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na kikundi cha Furaha ,wengine pichani ni Mbunge wa Urambo Masahariki Samuel Sitta,Mbunge wa Viti Maalum Magreth Sitta na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Fatma Mwassa.

This entry was posted in

Leave a Reply