Google PlusRSS FeedEmail

KINANA AWASILI NZEGA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa katika kijiji cha Ziba mpakani mwa wilaya ya Igunga na Nzega.
 Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tabora Munde Tambwe akiwasalimia wakazi wa Nzega mkoani Tabora wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bi. Fatma Mwassa akiwasalimia wananchi wa Nzega kwenye mpaka wa Nega na Igunga ambapo alijibu pia changamoto zilizotolea na wananchi waliomuuliza swali Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana juu ya ajali nyingi zinazotokea eneo hilo na kusababisha wanafunzi wengi kugongwa na magari, Mkuu wa Mkoa alisema Serikali itaweka alama za Barabarani ndani ya siku 14.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimia wakazi wa Nzega baada ya kupokelewa wakitokea wilaya ya Igunga ambapo walifanya ziara ya siku mbili.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wananchi waliojitokeza kwa wingi kumpokea kwenye mpaka wa Igunga na Nzega. Katibu Mkuu leo ameanza ziara ya siku mbili wilaya ya Nzega mkoani Tabora.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa wilaya ya Nzega Ndugu Hussein Bashe.Katibu Mkuu amepokelewa wilayani Nzega ambapo atakaa kwa siku mbili kujenga na kukiimarisha chama, kukagua miradi ya maendeleo na utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya 2010.

This entry was posted in

Leave a Reply