Google PlusRSS FeedEmail

KINANA AMALIZA ZIARA YAKE WILAYA YA MKALAMA KESHO KUHUTUBIA MKUTANO MKUBWA SINGIDA MJINI


  • Ahutubia Gumanga,Nduguti, Nkingu na Iguguno.
  • wananchi wapenda hotuba zake kwani nikiongozi pekee anayezungumzia maendeleo na ukweli mtupu .
  • Kesho kufanya mkutano mkubwa Singida mjini kwenye viwanja maarufu vya People's
  • Mkutano huo utarushwa moja kwa moja na televisheni ya Star Tv
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Nduguti wilaya ya  Mkalama na kuwaambia wananchi hao kuwa ahadi za Chama cha Mapinduzi zinatekelezwa na vijiji vingi vitapata umeme na vituo vingi vya afya ninajengwa sambamba na maabara katika sekondari za kata kote nchi nzima.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi akihutubia wakazi wa Nduguti na kuwaambia wilaya ya Mkalama itakuwa wilaya ya kimkakati na uchumi wake utakuwa mkubwa siku za mbele kuzidi hata Kiomboi kwani Barabara itakapokamilika na huduma zingie kuwa karibu maendeleo yatakuja kwa kasi zaidi wilayani hapo.
 Umati wa wananchi wa Nduguti wakifuatilia mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwa Makini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Gumanga
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Iguguno ambapo alielezea umuhimu wa Muungano na kuwataka watu kuwa makini na wanasiasa wnaojali vyeo kuliko umoja na mshikamano wetu.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimiminiwa uji wa ulezi nyumbani kwa balozi Fatma Kassim wa shina namba 5,Gumanga wilaya ya Mkalama mkoani Singida.
 Balozi wa Shina namba 5 Fatma Kassim (wa tatu kulia) akinywa uji wa ulezi pamoja na wageni zake Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida Ndugu Mgana Msindai.
 Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Mwigulu Nchemba akinywa uji wa ulezi nyumbani kwa Balozi wa shina namba 5 pamoja na Mbunge wa Viti Maalum wa mkoa wa Singida Ndugu Martha Mlata na Mlezi wa CCM mkoa wa Singida Bi.Hadija Aboud ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa (Zanzibar)
 Ujumbe wa kata ya Gumanga,wilaya ya Mkalama Mkoa wa Singida .
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia moja ya nguzo za Daraja linalojengwa mto Sibiti, wilaya ya Mkalama mkoani Singida ,daraja hilo likikamilika litasaidia sana kukua kwa wilaya ya Mkalama .

This entry was posted in

Leave a Reply