Google PlusRSS FeedEmail

KINANA AWASILI WILAYA YA BABATI VIJIJINI


Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Ndugu Vrajilal JituSon mara baada ya kuwasili na kupokelewa katika Kata ya Magara wilaya ya Babati Vijijini.Katibu Mkuu wa CCM yupo ziarani katika mkoa wa Manyara ambapo atafanya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kukagua uhai wa chama.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwa amezungukwa na wakazi wa Kata ya Magara wilayani Babati Vijijini waliojitokeza kwa wingi kuwapokea mara baada ya kuwasili wilayani hapo .
 Wananchi wa Kata ya Magara wakiwa na nyuso za furaha wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana  ambaye ameongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimu wananchi wa kata ya Magara kabla ya kukagua mradi wa ujenzi  wa wodi ya kituo cha afya cha Mama na Mtoto.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini Ndugu Vrajilal JituSon mara baada ya kukagua mradi wa ujenzi wa wodi ya kituo cha afya cha mama na mtoto.Katibu Mkuu wa CCM yupo ziarani katika mkoa wa Manyara ambapo atafanya shughuli za kimaendeleo ikiwemo kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kukagua uhai wa chama.
 Wananchi wa Kijiji cha Magara wakionyesha bango la kuomba msaada wa kusaidiwa kujengwa kwa daraja katika mto Mangara.
 Mto Magara ambao wananchi wanaomba daraja lijengwe.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akihutubia wakazi wa kata ya Magugu ambapo aliwapa usia vijana wenzake kwa kuwaambia Vijana wachape kazi na waachane na talalila za wanasiasa njaa.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa  Magugu na kuwaambia viongozi wengi wa vijiji wamekuwa wakiingia mikataba bila kuwashirikisha wananchi hivyo kusababisha migogoro mikubwa ya ardhi na amewataka wananchi kuchagua viongozi makini,Katibu Mkuu wa CCM ameshtushwa na baadhi ya watu kumiliki sehemu kubwa ya ardhi na kuwakodishia wananchi kwa ajili ya kilimo cha mpunga.

This entry was posted in

Leave a Reply