Google PlusRSS FeedEmail

KINANA ATINGA URAMBO KUFANYA ZIARA YA SIKU MOJA


 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Urambo Ndugu  Samuel Sitta wakati wa mapokezi katika kijiji cha Izimbili wilaya ya Urambo mkoani Tabora,Katibu Mkuu atakuwa kwenye ziara ya siku moja katika  wilaya ya  Urambo ambapo atakagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010 na uhai wa Chama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mbunge wa Viti maalum mkoa wa Tabora Magreth Sitta wakati wa mapokezi katika kijiji cha Izimbili wilaya ya Urambo mkoani Tabora,Katibu Mkuu wa CCMatakuwa kwenye ziara ya siku moja katika  wilaya ya  Urambo ambapo atakagua utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010 na uhai wa Chama
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasalimia wakazi wa kijiji cha Izimbili wilayani Urambo mkoa wa Tabora.

 Umati wa wananchi wa kijiji cha Izengabatogilwe ukiwa nje ya jengo la Zahanati,Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alitembelea zahanati hiyo na kukagua maendeleo ya zahanati hiyo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na wananchi wa kijiji cha Izengabatogilwe wakati wa ukaguzi wa mradi wa zahanati ya kijiji hicho.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua vyumba vya zahanati ya kijiji cha Izengabatogilwe


Zahanati ya kijiji cha Izengabatogilwe
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa maabara ya shule ya sekondari ya Uyumbu akishirikiana na Mbunge wa Urambo Ndugu Samuel Sitta.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na kikundi cha ulinzi shirikishi cha kijiji cha Izengabatogilwe pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye na mbunge wa Urambo Ndugu Samuel Sitta.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua shamba la mahindi kwenye Mradi wa Shamba Darasa kituo cha kilimo cha Matone katika kijiji cha Kapilole ,Urambo.
 Shamba la mahindi katika kituo cha Kilimo cha matone katika kijiji cha Kapilole,Urambo.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa kwenye picha ya pamoja na wakulima kituo cha Kilimo cha Matone,wengine pichani ni Mbunge wa Urambo Ndugu Samuel Sitta na Mbunge wa Viti Maalum Magreth Sitta.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa ofisi ya CCM Tawi la Mabatini pamoja na Mbunge wa Urambo Ndugu John Samuel Sitta na wana CCM wengine.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia vitanda vya wodi ya Mama Ngojea kwenye hospitali ya wilaya ya Urambo,ambapo wodi hiyo itasaidia sana wakina mama kujifungua salama.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini vitabu vya wageni kabla ya kuanza kwa kikao cha halmashauri kuu ya  CCM wilaya  ya Urambo,wengine pichani ni Mbunge wa Urambo  Samuel Sitta na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Wajumbe wa Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM wilaya ya Urambo wakiwa kwenye ukumbi wa mkutano tayari kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.

This entry was posted in

Leave a Reply